Search This Blog

Tuesday, February 14, 2012

TEVEZ ARUDI ENGLAND - AGOMA KUOMBA SAMAHANI NA KUWAITA VIONGOZI WA CITY NA MANCINI WAONGO.


Carlitos akiwasili jijini Manchester leo hii.



Muda mchache baada ya kurudi England, Carlos Tevez amemtuhumu Roberto Mancini kwa kumtendea mambo ambayo hata mbwa hafai kutendewa na amembandika kocha huyo wa kiitaliano jina la “Muongo”.

Tevez amerudi leo Manchester baada ya kugoma kwa muda wa miezi 3.
Carlitos alimlipukia Mancini akiwa anakumbuka usiku wa mechi dhidi ya Bayern wakati Mancini alipogombana na Edin Dzeko, then akamfuata Muargentina huyo.
Tev alisema: “ Alikuwa katikati ya majibizano na Dzeko, akaniambia mie niendelee kupasha na kunitendea mambo ya kinyama na kitumwa.
Carlos Tevez akiingia katika mako makuu ya Manchester City.



“Alipoendelea kunisemesha kwa sauti ile kama anaongea na mbwa ndipo nilipomwambia sitofanya warm up.”
“Nilikuwa radhi kucheza lakini kocha alikuwa katika mood ya kijinga kwa sababu alikuwa anagombana na Dzeko. Pia baada ya Dzeko akanifuata mimi huku akitoa maneno machafu dhidi yangu, na muda wote huo nilikuwa mkimya.”

Pia Tevez alizungumzia juu uongo alioutoa Mancini katika kikao cha bodi ya Man City kuhusu kilichotokea usiku ule.


“Niliwaambia Man City, mimi ni mwajiriwa wa City inabidi mnithamini. Mancini amesema uongo kuhusu mimi na wakurugenzi wa Man City wanajua juu ya hili.
“Wanampendelea Mancini. Nataka City wawambie ukweli mashabiki.”

City na Mancini walikuwa na matumaini Carlitos angeitumia interview hii kuomba samahani na kuweka mambo sawa kati yake na klabu pamoja na kocha.

No comments:

Post a Comment