Search This Blog

Tuesday, February 14, 2012

PAUL SCHOLES YUPO TAYARI KURUDI KUICHEZEA ENGLAND - REDKNAPP AKIWA KOCHA.




Mwezi mmoja baada ya kuhairisha uamuzi wake wa kustaafu na kurudi uwanjani kuitumikia klabu yake ya Manchester United, Paul Scholes sasa yupo tayari kurudi pia katika timu ya taifa ya England katika michuano ya EURO 2012.

Habari hizi zimekuja wakati England ikiwa katika wakati mgumu baada ya sakata la Terry lilopelekea kujiuzulu kwa kocha Fabio Capello.

Lakini pia uamuzi huu Scholes utakuwa mzuri mno kwa kocha atakayepewa jukumu la kuiongoza England in EURO.
Harry Redknapp, kocha anayepewa nafasi kubwa kumbadili Fabio Capello alikiri wiki iliyopita kuwa kama atakuwa kocha wa Three Lions basi atamchagua Scholes katika kikosi chake.

Na kiungo huyo mwenye miaka 37, ambaye alikataa wito wa Capello alipoitwa wakati wa kombe la dunia 2010, anaripotiwa kuwa yupo tayari kurudi dimbani kuisadia England kushinda kikombe cha ulaya kipindi kijacho cha kiangazi.

Scholes alicheza mechi yake ya mwisho ya kimataifa miaka 8 iliyopita wakati England ilipotolewa na Portugal katika michuano ya EURO 2004 kwa mikwaju ya penati.
Inasemekana aliamua kustaafu mapema baada ya kuwa frustrated kwa kuchezeshwa namba ambayo hakuipenda huku akiunda partnership ambayo haikuwa na mafanikio kati yake na Frank Lampard na Steven Gerrard.

Lakini majuto ya kukosa kucheza World Cup 2010 in South Africa ndio inasemekana sababu kubwa ya Scholes kuwa tayari kurudi dimbani kwa ajili ya kuitumikia kwa mara ya mwisho Three Lions.
Ikiwa Redknapp atachaguliwa kuwa kocha wa England, then tutegemee kumuona fundi Scholes ndani ya kikosi cha wachezaji 23 watakaounda kikosi cha Euro 2012.
Kiongea kuhusu Scholes Harry alisema: “Mwangalie Paul Scholes, na tuwe wakweli, kama kocha ni lazima upende kuwa na mchezaji wa aina yake katika michuano mikubwa kama Euro.”

No comments:

Post a Comment