Search This Blog

Wednesday, February 29, 2012

SIMBA TV KUZINDULIWA RASMI IJUMAA

KLABU ya soka ya Simba inatarajiwa kufanya hafla ya uzinduzi wa Simba Tv ambao unatarajiwa kufanyika Ijumaa katika hoteli ya JB Belmont iliyopo katika jengo la Benjamin Mkapa katikati ya jiji la Dar es Salaam.
Ofisa habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga amesema kwamba Simba Tv itakuwa ikirushwa katika kituo cha Clouds Tv.
Alisema kupitia uzinduzi huo kutakuwa na burudani mbalimbali sambamba na kuonyeshwa kwa documentary maalum inayohusu klabu hiyo.
"Hafla hii itakuwa ni kwa waalikwa huku wengine watakaopenda kuhudhuria watapaswa kulipa shilingi 70,000.

No comments:

Post a Comment