Search This Blog

Friday, February 10, 2012

PATRICK VIEIRA: WAAMUZI HAWATAKI CITY TUCHUKUE UBINGWA WA ENGLAND




Patrick Vieira amewabwatukia marefa wa premier league na kusema kwamba wana agenda ya siri ya kuhakikisha Manchester City hawachukui ubingwa wa English premier league.
Vieira, ambaye ni mkurugenzi wa kitengo cha ukuzaji vipaji cha Manchester City, anaamini vijana wa Roberto Mancini wamekuwa wakitendewa visivyo na marefa katika siku za hivi karibuni.

City walimpoteza nahodha wao Vincent Kompany na mshambuliaji Mario Balotelli waliofungiwa kwa mechi 4 kila mmoja huku wakiwa wapo mbele kwa pointi 2 mahasimu wao Manchester United.


Kompany alitolewa nje kwa kufanya tackle ya miguu miwili dhidi ya Nani wakati wa mechi ya kombe la FA dhidi ya Manchester United lakini Vieira aliitolewa mfano tackling ya ya Frank Lampard dhidi ya Adam Hammill wa Wolves na mwisho wa siku star huyo wa Chelsea alipata kadi ya njano tu.

Balotelli aliadhibiwa baada ya kumkanyaga kwa makusudi kiungo wa Spurs Scott Parker  na pia hapo tena Vieira amesema Peter Crouch alifanya hivyo kwa mchezaji Jonas Olssson lakini hakuadhibiwa.


‘Sipendi kufikiria kuhusu jambo hili kwa sababu sitaki kusema kila mtu haipendi City au jambo lolote la namna hiyo.

‘Lakini unapoangaliwa katika maamuzi ya hivi karibuni, unajiuliza mwenyewe kama kuna tatizo lolote dhidi yetu, au hawataki City tuchukue ubingwa. Vieira aliongeza” “Tackle ya Lampard ilikuwa inaonekana hatari mno ukilinganisha nay a Vincent, au namna Peter Crouch alipomuingiza vidole machoni mpinzani wake, ilikuwa hatari zaidi.

“Tunajitahidi kufanya vizuri tushinde kombe, tunakuabli adhabu zetu, lakini unapoangalia matukio yanayolingana yanapotolewa maamuzi tofauti, unahisi kuonewa na inaudhi sana hali hiyo.”

No comments:

Post a Comment