Search This Blog

Sunday, February 12, 2012

BAADA YA OSAMA, STEVE JOBS, GADDAFI - AARON RAMSEY APIGA BAO NA WHITNEY AFARIKI


Ni ajabu lakini ndio ukweli, imekuwa ikitokea kila siku ambayo mchezaji wa Arsenal Aaron Ramsey anapofunga bao kwa timu yake ya Gunners basi kuna tukio la kifo cha mtu mashuhuri duniani kitatokea.

Alianza alipofunga goli siku ya May 1 2011dhidi ya Manchester United katika mechi ambayo Arsenal walishinda, masaa machache baada ya mechi dunia ilitangaziwa kuwa Gaidi namba 1 Osama Bin Laden aliuwawa.

Kwa mara nyingine tena Ramsey akafunga bao katika mechi dhidi ya Spurs tarehe 2 mwezi wa 10, 2011 na siku chache baadae mmiliki wa kampuni ya APPLE Steve Jobs akafariki dunia.

Baadae tarehe 19 October 2011 Ramsey akaifungia Arsenal goli dhidi ya Marsaille – masaa machache baadae tukatangaziwa kuuwawa kwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.
Na jana tarehe 11/2/2012 Aaron Ramsey alifunga bao la kuongoza kwa Arsenal katika mechi ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Sunderland – na masaa machache baadae mjini Baverly Hills – USA sanaa ya muziki imekumbwa na masikitiko makubwa baada ya kuondokewa na mwanamuziki Whitney Houston.

1 comment:

  1. Kaka hii ni hatari,jamaa ana uhusiano na fremason nini? Hii ni record ya aina yake,kazi njema.I'm Keny Mgaya from Arusha.

    ReplyDelete