Search This Blog

Friday, February 10, 2012

ADRIANO AFUNGIWA HOTELINI NA KLABU YAKE KWA AJILI YA DIET YA KUPUNGUZA UNENE.


BONGE ADRIANO AKISHANGILIA BAADA YA KUFUNGA GOLI KATIKA MECHI MOJAWAPO ALIZOCHEZA.
Alikuwa mshambuliaji wa kutisha enzi zake, na mshindi wa mara nne wa Scudetto akiwa na Inter Milan, Adriano Leite Ribeiro alikuwa moja ya washambuliaji walionekana kuwa wamekuja kumrithi El Phenomena Ronaldo De Lima.

Kama isingekuwa kwa kupenda kwake maisha ya starehe na kujirusha, angeweza leo hii kuwa amekaribia au kupita mafanikio ya wachezaji wenzie kama Ronaldo au Ronaldinho, lakini mambo yamezidi kumuendea kombo Adriano na akaamua kurudi kucheza nyumbani kwao Brazil.

Kibonge Ronaldo amkaribisha Adriano baada ya kusajiliwa na timu hiyo last season.
Sasa akiwa nyumbani @Corinthians, uzito wa mwili wa Adriano umekuwa kikwazo na tatizo kubwa kwa klabu yake, sasa wameamua kumfungia mchezaji huyo katika chumba cha hotel na kumpa chakula ambacho kitakuwa kimepitishwa na daktari wa timu hiyo.

Msemaji wa Corinthians Fabio Mahseredjian alisema: “Akiwa hotelini tumeweza zaidi katika kum-control. Anajua tunafanya haya yote kwa ajili yake ili aweze kufanya vizuri. Sisi sote tumejitolea kufanya haya, lakini yote inategemea nay eye. Kupunguza uzito kunawezekana kwa kufanya diet nzuri tu, huwezi kupunguza uzito kwa kufanya mazoezi pekee.

 

1 comment:

  1. hapa bongo wachezaji wafungiwe ili wasinyew viroba maana kwao vimekua icream ndo maana hawana stamina we viroba afu sembe na bamia wapi nawapi

    ReplyDelete