Search This Blog

Saturday, January 28, 2012

YANGA WAWAPIGISHA KWATA WANAJESHI WA JKT RUVU: WAWATANDIKA 3-1


Alikuwa mshambuliaji na mchezaji bora wa Uganda, Hamisi Kiiza aliyeokoa jahazi la mabingwa wa Tanzania Bara Yanga kutokomea kwenye gwaride la JKT Ruvu kabla ya Mwasika kuipoteza JKT Ruvu.

Katika mchezo huo wa ligi kuu ya vodacom uliochezwa katika uwanja wa Taifa, JKT Ruvu walikuwa wa mwanzo kupata goli katika dakika ya 33 kupitia kwa Amos Mgisa.

Kama yanga wangekuwa makini wangekwenda mapumziko wakiwa mbele kwa goli 2 ama zaidi, lakini walikwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa goli moja huku wakipoteza nafasi walizopata kupitia kwa Kenneth Asamoah.

Yanga iliwabidi wangoje mpaka dakika ya 60, ambapo walisawazisha goli kupitia kwa Hamisi Kiiza kwa Mkwaju wa penati, na dakika 19 mbele Kiiza alirejea tena nyavuni kwa kuifungia Yanga goli la pili.

Wakati JKT Ruvu wakiwa wanajiuliza kilicho wasibu walijikuta wanatundikwa msumari wa tatu katika dakika ya 89 kupitia kwa Stephan Mwasika, hivyo kuwaashia indiketor Simba waliopo kileleni.


Katika mchezo mwingine wa ligi kuu uliochezwa Mlandizi ulimalizika kwa sare ya goli 1-1 pale Ruvu shooting ulipo wakaribisha Kagera Sugar.

Katika mchezo huo magoli yote yalifungwa katika kipindi cha kwanza, huku Ruvu Shooting wakiwa wa mwanzo kupata goli katika sekunde ya 33 kupitia kwa Abdurahman Abdurahman.

Kagera Sugar walikuja kusawazisha goli hilo katika dakika ya 26, na kupelekea mchezo kuisha kwa sare ya goli 1-1.


Katika uwanja wa Azam, Toto Africa imekubali kupokea kichapo cha pili mfululizo toka kwa Villa Squad inayoangaika kujinasua toka mkiani, wakati jahazi la Toto likiendelea kuzama.

Magoli ya mshambuliaji wazamani wa Moro united na Yanga Nsa Job na Makundi yalitosha kuwapa point 3 muhimu Villa Squad na kuibuka na ushindi wa magoli 2-0.

MSIMAMO WA VPL.
Kwenye Mabano Idadi ya Mechi Zilizochezwa.
1. Simba SC (14) 31
2. Yanga (15) 31
3. JKT Oljoro (14) 26
4. Azam FC (14) 26
5. Mtibwa Sugar (14) 22
6. Kagera Sugar (15) 20
7. JKT Ruvu (15) 17
8. Ruvu Shooting (15) 17
9. Moro United (14) 15
10. African Lyon (14) 14
11. Toto Africa (15) 13
12. Polisi Dodoma (14) 12
13. Coastal Union (14) 11
14. Villa Squad (15) 10

Aboodmsuni.blogspot.com

No comments:

Post a Comment