Search This Blog

Friday, January 13, 2012

USAJILI WA YANGA, SIMBA WAPITA CAF

Wachezaji wote wa klabu za Yanga na Simba walioombewa usajili Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kwa ajili ya michuano ya Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho umepita. Klabu hizo ziliombea wachezaji 28 kila moja. Hata hivyo Simba ambayo itacheza Kombe la Shirikisho awali iliombea usajili wachezaji 26 kabla ya baadaye kuwaongeza Ulimboka Mwakingwe na Derreck Walulya. Katika michuano hiyo Yanga imepangiwa Zamalek ya Misri ambapo itaanzia nyumbani wakati Simba itaanzia ugenini jijini Kigali, Rwanda kwa kuikabili Kiyovu Sport ya huko.

No comments:

Post a Comment