Search This Blog

Sunday, January 29, 2012

TWIGA STARS YAITANDIKA NAMIBIA MABAO 5-1

Timu ya Taifa ya Wanawake ya Soka Twiga Stars wamewasambaratisha Namibia kwa jumla ya magoli 7 kwa 2 na sasa wanawangoja kati ya Misri ama Ethiopia ambapo mchezo wa kwanza Misri walishinda goli 4-2.

Katika mchezo wa leo ambapo Twiga Stars wameibuka na ushindi wa goli 5-2 katika uwanja wa Taifa huku wa Namibia wakienda huku wakimkumbuka mshambuliaji alivaa jezi namba 8 Mwanahamisi Omary, kwanamna alivyokuwa wanawaenyesha mabeki wa timu hiyo.

Twiga Stars walianza kuandika goli la kwanza katika dakika ya 22 kupitia kwa Mshambuliaji Hatari na mwenye kasi Mwanahamisi Omar.

Goli hilo halikukaa sana kwani katika dakika ya 30 Albert Dakisi aliisawazishia goli hilo kwa mpira wa kona na yeye kuiunga kwa kichwa na mpira kutinga moja kwa moja nyavuni. Na kupelekea timu kwenda mapumziko wakiwa sare ya goli 1-1.

Katika kipindi Cha pili Mwanahamisi Omari aliyekuwa ana ama kila upande alimpa pasi murua Asha Rashidi katika dakika ya 47, ambapo Asha akufanya ajizi na kuundumbukiza mpira wavuni.

Baada ya goli hilo Namibia walikuja juu huku ukuta wa Twiga ukifanya makosa ya hapa na pale lakini Namibia walishindwa kuyatumia mpaka katika dakika 72, ambapo mpira ulidundishwa chini na mwamunzi ndani ya eneo la hatari ya Twiga stars baada ya Mwanahamisi Omary kuwa chini, wakati Twiga wakitegemea Namibia wangecheza fair play kwa kutoa mpira nnje mambo yalikuwa tofauti, kwani alitoa pasi ya goli huyo mchezaji wa Namibia na kuipatia goli la 2 Namibia.

Mwanahamisi Omari aliendeleza usumbufu wake safari hii akitokea kushoto, upande uliokuwa dhaifu kwa Namibia hii leo, kwa kuwalamba chenga mabeki wa Namibia na Kipa wake lakini mpira wake ulizuiwa na mlinzi na kumkuta Eto'o Mlenzi na kuifungia Twiga goli la 3 katika dakika ya 84.

Goli hilo liliwafanya Twiga kucheza soka safi na dakika ya 88 Asha Rashidi aliipatia Twiga Stars goli la 4 na la 5 likifungwa na Mwanahamisi Omari katika dakika 90 na mchezo kumalizika kwa Twiga kushinda goli 5-2.

Kwa ushindi huo Twiga Stars imeitoa Namibia kwa jumla ya goli 7-2 hivyo wanangoja mshindi kati ya Misri na Ethiopia. Na endapo wakishinda mchezo huo utakao chezwa mei watakuwa wamefuzu kwa mara ya pili mfululizo katika michuano ya 8 ya mataifa ya Africa itakayo fanyika Equaterial Guinea hapo november mwaka huu.

No comments:

Post a Comment