Search This Blog

Wednesday, January 11, 2012

SHWEINSTEIGER: XAVI NA INIESTA NI BORA DUNIANI


Siku moja baada ya Lionel Messi kutangazwa kuwa mchezaji bora wa dunia, kiungo wa Bayern Munich Bastian Schweinsteiger amesema anaamini kuwa viungo wa Barcelona Xavi na Andres Iniesta ndio wachezaji bora wa dunia kwa mujibu wake.

Nahodha huyo msaidizi wa Ujerumani kwa siku za hivi karibuni amekuwa akifananishwa na majembe hayo mawili ya Barcelona na Spain akiongea na mtandao wa Goal com, alisema Xavi na Iniesta wana uwezo mkubwa na amedhamiria kujituma mpaka kufikia uwezo wao.

“Xavi na Iniesta ni wachezaji wa mfano wa kuigwa. Wanacheza katika timu bora ya dunia. Na tutajaribu kuweza kupambana kufikia uwezo wao na kuwashinda. Endapo tutawafunga Barcelona basi hapo ndipo baadhi ya wachezaji wa Bayern wanaweza kuonekana kama wachezaji bora.”

No comments:

Post a Comment