Search This Blog

Wednesday, January 11, 2012

HENRY: NATAKA KUWAKOMESHA SPURS KABLA SIJAONDOKA EMIRATES


Thierry Henry anataka kuwaadabisha Tottenham Spurs kabla hajaondoka Arsenal na kurudi Marekani.

The French striker, 34, currently anacheza kwa mkopo @Emirates mpaka mwezi wa pili tarehe 16, akiwa na uhuru kuongeza siku za kukaa mpaka siku nyingine 10.

Kitu ambacho kitampa nafasi ya kucheza North London derby dhidi ya Tottenham tarehe 26 mwezi ujao.

Henry alisema: “ Itakuwa ndoto kucheza mechi hiyo dhidi ya Spurs. Yote inategemea jinsi kocha atakavyoamua ni kwa muda gani nitakuwepo hapa.

“Msisahau kuwa mimi bado mchezaji wa New York na kuwa nahodha pia kunaniongezea majukumu mengine ambayo napaswa kuyaheshimu.

“Kwa hakika nitakuwa bado nipo hapa kwa mchezo dhidi ya Manchester United na pia ningependa kucheza mechi ya Champions league dhidi ya AC Milan, ingawa sifikirii kama nitakuwepo hapa katika mchezo dhidi ya Tottenham kwasababu nitakiwa nirudi New York kujiandaa na msimu mpya."

No comments:

Post a Comment