Search This Blog

Friday, January 13, 2012

INTER YAMRUDIA CARLOS TEVEZ

Inter Milan wapo tayari kufungua upya mazungumzo na Manchester City juu ya Carlos Tevez baada ya mahasimu wao AC Milan kujitoa katika mazungumzo kwa ajili ya kumsajili muargentina huyo.

Mapema wiki hii Raisi wa Inter Milan Massimo Morati alisema wameshindwa kupambana na Milan katika harakati za kumsaini Tevez, lakini hiyo ilikuwa kabla ya makamu wa raisi wa Milan Adriano Galliani kujitoa katika mazungumzo na City baada ya Alexandre Pato kukataa kujiunga na PSG.

Huku mustakabali wa Tevez ukiwa bado haupo sawa, Morrati yupo tayari kurudi katika meza ya mazungumzo na City.

Mbele ya mchezo wa derby wiki hii Morrati aliwaambia waandishi wa habari, “Sisi na City wote tunajua yote kuhusu hali ya Tevez lakini tumeamua kuhairisha mazungumzo hadi wiki ijayo, kwa kuwa sasa attention yote ipo katika mchezo wa Jumapili.”

No comments:

Post a Comment