Search This Blog

Friday, December 16, 2011

LIGI YA ‘MO’ KUANZA KUTIMUA VUMBI JUMAPILI MKOANI SINGIDA

Na.Nathaniel Limu.

Ligi maarufu ya kombe la mbunge wa jimbo la Singida mjini Mh. Mohammed Gullam Dewji inatarajiwa kuanza kutimua vumbi kuanzia tarehe 18/12/2011 kwenye uwanja wa Namfua mjini Singida.
Kwa mujibu wa mratibu wa ligi hiyo Katibu wa mbunge Dewji Duda Mughenyi, jumla ya timu 16 za soka za kata ya Manispaa ya Singida zitashiriki ligi hiyo.
Duda amesema Mh. Dewji ametoa jezi 240, mipira 53 na soksi 240 ambapo kila kata imepata jezi pea 15 na soksi 15 kwa ajili ya kufanikisha maandalizi ya kushiriki ligi.
Amesema timu hizo za kata ambazo hazina chembe chembe yo yote ya itikadi ya kisiasa, udini, ukabila, wala rangi, zimegawanywa katika makundi manne ambapo kila kundi litakuwa na timu nne.
Duda amesema kundi A, litakuwa na timu za kata ya Mitunduruni, Ipembe, Utemini na Minga, Kundi B, Majengo, Kindai, Mughanga na Misuna, Kundi C, Unyambwa, Mandewa, Mtipa na Uhamaka na kundi D, Litakuwa na timu ya kata ya Mtamaa, Mungumaji, Unyamikumbi na Mwankoko.
Amesema ligi hiyo inayotarajiwa kumalizika Januari 21 mwakani, mechi ya fungua dimba ambayo itachezwa Jumapili Desemba 18 mwaka huu, itazikutanisha timu za Mitunduruni na Utemini.
"Mshindi wa kwanza, atapata kombe kubwa hadhi ya dhahabu na shilingi laki moja taslimu, wa pili atapata kombe dogo na shilingi laki mbili, wakati yule wa tatu, atazawadiwa shilingi laki moja", amesema Duda.
Akizungumza kenye hafla ya kugawa vifaa vya michezo ya ligi hiyo, Katibu mpya wa CCM Manispaa ya Singida, Magdalena Ndwete, amewataka wachezaji wa timu hizo, kuheshimu sheria 17 za soka, ili kudumisha amani na utulivu wakati wote wa ligi hiyo.
"Mkifanya hivyo, lengo la mbunge wetu Dewji la kukuza vipaji vyenu, kuwasaidia kujitangaza, kujenga afya na kupanua wigo wa marafiki, litafikiwa kwa ufanisi mkubwa” amesema.
Kwa upande wa waamuzi wa ligi hiyo, Ndwete, amewataka wasijihusishe na vitendo vitakavyochangia kuvuruga ligi hiyo vikiwemo vya upendeleo na uonevu.


Msaidizi wa mbunge Mohammed Dewji Duda Mughenyi akishiriki kugawa vifaa vya michezo kwa ajili ya ligi ya Mo. (Picha zote na Nathaniel Limu).






Vikombe vitakavyoshindaniwa kwenye ligi ya kombe la mbunge wa jimbo la Singida mjini Mh. Mohammed Dewji.





Katibu wa CCM manispaa ya Singida Magdalena Ndwete akionyesha jezi zitakazotumiwa wakati wa ligi ya kombe la mbungeMh. Mohammed Dewji




Katibu wa CCM manispaa ya Singida akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi vifaa vya michezo vilivyotolewa na mbunge wa jimbo la Singida mjini Mh. Mohammed Dewji.

1 comment:

  1. kinachoniudhi mimi,ni wanasiasa kugeuza football kama forum ya kuwapoza wananchi wao na machungu na kuacha kushughulikia mambo ya msingi,kazi yao ni kutetea maslahi yetu huko bungeni sio kugeuka wafadhili wa vitu vidogo vidogo ambavyo sio ishu,nini mipira na jezi?wanatuharibia mpira wetu,chela wa dom

    ReplyDelete