Search This Blog

Tuesday, December 6, 2011

KILIMANJARO STARS YATINGA NUSU FAINALI CECAFA CUP

Timu ya taifa ya Tanzania bara Kilimanjaro Stars imefanikiwa kuingia nusu fainali ya CECAFA Senior Challenge Cup 2011, baada ya kuifunga timu ya Malawi kwa goli moja kwa bila. Goli la Stars lilifungwa na kiungo Nurdin Bakary katika kipindi cha kwanza na kudumu mpaka mwisho wa mchezo.

Kwa matokeo hayo Kili stars sasa itacheza na Uganda katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali siku ya Alhamisi.


No comments:

Post a Comment