Search This Blog

Thursday, October 6, 2011

SIMBA DIMBANI NA PRISONS JUMAMOSI

Siku ya jumamosi ya wiki hii, vinara wa ligi kuu Tanzania Bara, Simba watacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu inayohangaika kusaka nafasi ya kurejea ligi kuu Tanzania Prisons ya Mbeya.

Mchezo huo wakirafiki utachezwa katika uwanja wa Azam uliopo Chamanzi nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.

Prisons ilishuka daraja katika msimu wa 2009/2010, baada ya kupata mafanikio katika msimu wa 2007/2008 kwa kushika nafasi ya pili na hivyo kupata nafasi ya kuiwakilisha nchi katika michuano ya Kombe la Kagame na Kombe La Shirikisho, ambapo hawakufua dafu baada ya kutolewa katika hatua za awali.

Prisons inajianda na michezo ya ligi daraja la kwanza ambao inatarajiwa kuanza kutimua vumbi oktober 15, wakati Simba wanajianda na muendelezo wa michezo ya ligi kuu ya vodacom.

No comments:

Post a Comment