Search This Blog

Thursday, October 6, 2011

SHAKIRA AKANUSHA KUACHANA NA PIQUE

Siku chache baada ya taarifa kuenea katika vyombo vya habari mbalimbali kuwa mapenzi kati ya Gerard Pique na mwanamuziki Shakira yamefikia tamati, leo mwanadada huyo kutoka nchini Colombia amekanusha kuachana na beki huyo wa kati wa klabu bingwa ya ulaya na timu ya taifa ya Spain.

The WakaWaka superstar alimtumia msemaji wake rasmi kutoa taarifa kuwa wawili hao bado wapo pamoja na taarifa kuwa wameachana ni uongo.

“Bado wapo pamoja na wanaendelea vizuri,” alisema msemaji huyo wa Shakira, bwana Rodrigo Beltran.

Mwanadada Shakira pia nae alitumia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter kumtakia heri mpenzi wake na timu ya taifa ya Spain katika mchezo wao kugombea nafasi kucheza michuano ya ulaya dhidi ya Czech Republic.

Aliandika “Good luck to the Spanish team this week and to my No. 3, muah! @3gerardpique.”

No comments:

Post a Comment