Search This Blog

Saturday, October 22, 2011

PHOTOS: KIKAO CHA VILABU 14 KILICHOAMUA LIGI KUU KUENDESHWA NA KAMPUNI.




Baada ya kikao cha karibia masaa 4 au zaidi viongozi wa vilabu 14 vinavyoshiriki ligi kuu ya Tanzania bara walifikia maamuzi ya kuanzishwa kwa kampuni itayoendesha ligi kuanzia msimu ujao.

Kikao hicho kilichofanyika katika hoteli ya JB Del-monte (zamani Paradise) @ Benjamin Mkapa Tower kilihudhuriwa na viongozi 13 kati ya 14 wa vilabu vya ligi kuu isipokuwa Kagera Sugar waliotoa udhuru lakini wakisema wataunga mkono maamuzi yatakayotolewa

Katika kikao hicho maamuzi yaliyotolewa ni kwamba uanzishwe mchakato wa kuwezesha usajili wa kampuni ambayo itaendesha ligi hiyo, huku Makamu mwenyekiti wa Simba Godfrey Nyange Kaburu akiteuliwa kuwa mwenyekiti wa kamati hiyo, Celestine Mwesiga katibu mkuu Yanga-Makamu mwenyekiti, Meja Ruta wa Ruvu Shooting- akiteuliwa Katibu wa hiyo kamati, na Shani wa Azam FC na Evadius Mtawala wa Simba wakiwa wajumbe, ambao wote kwa pamoja watashugulikia mchakato wa kupatikana kwa usajili wa kampuni hiyo.

“Dauda nilialikwa na viongozi wa vilabu kutoa mawazo yangu juu mchakato mzima wa kuundwa kwa kampuni itayoendesha ligi kuu.”

Pia viongozi hao wa vilabu 13 vya ligi kuu walitoa shukrani sana kwa vyombo vya habari hususani kwa watangazaji wa vipindi vya Sports extra na Sports Bar kutoka Clouds media group kwa kuwa watu wa kwanza kuanzisha na kusimamia mjadala wa kuanzishwa kwa kampuni ya kuendesha ligi kuu Tanzania bara.

No comments:

Post a Comment