Search This Blog

Wednesday, October 19, 2011

NGORONGORO HEROES YAPANGWA NA SOUTH AFRICA COSAFA CUP

Timu ya taifa chini ya miaka 20 Ngorongoro Heroes ipangwa kundi C pamoja na South Africa katika michuano ya vijana ya COSAFA itakayofanyika nchini Botswana.

Ngorongoro heroes itashiriki kama timu mualikwa katika mashindano hayo yanayohusisha timu za Taifa za vijana chini ya miaka 20 kwa mataifa ya kusini mwaafrica.

Ngorongoro wamepangwa kundi C pamoja na South Africa, Zambia, na Mauritius, wakati kundi A lina timu za Botswana, Comores, Swaziland na Mozambique.

Kundi B lina timu toka Seychelles, Malawi, Lesotho na Zambia na Kundi D lina timu za Angola, Madagascar, Namibia na Zimbabwe.

Mashindano hayo yanatarajiwa kuanza december 01 mwaka huu kwa mchezo kati ya Botswana na Comores, wakati Swaziland ikiwakabili Mozambique siku hiyo ya ufunguzi.

Ngorongoro watafungua kwa kucheza na Zambia december 2 wakati Angola wakicheza na Madagascar, Namibia na Zimbabwe, South Africa na Mauritius, Seychelles na Malawi siku hiyo.

RATIBA YA MICHEZO MENGINE.

4/12/2011
Malawi vs Lesotho
Comores vs Swaziland
Mozambique vs Botswana
Tanzania vs South Africa
Mauritius vs Zambia

05/12/2011
Madagascar vs Namibia
Zimbabwe vs Angola
Lesotho vs Seychelles

06/12/2011
Madagascar vs Zimbabwe
Tanzania vs Mauritius
Comores vs Mozambique
Namibia vs Angola
South Africa vs Zambia
Swaziland vs Botswana

08/12/2011: SEMI FINALS
Winner A vs Winner C
Winner B vs Winner D


10/12/2011:
FINAL

No comments:

Post a Comment