Search This Blog

Wednesday, October 5, 2011

MAGOLI YA HATARI KUWAHI KUFUNGWA KWENYE KOMBE LA DUNIA.

WORLD CUP NA MAGOLI MAKALI

10: Pele (Brazil) vs Sweden @Sweden 58

Goli la Gazza dhidi ya Scotland sio kali kihivyo.Imekuja kufahamika amelikopi kutoka Pele ambaye alifunga goli kama hilo katika fainali za kombe la dunia nchini Sweden mwaka 1958.



9:Diego Maradona (Argentina) vs Greece @USA 94

Maradona aliushangaza ulimwenguni alipoondolewa katika mashindano ya mwaka 1994 baada ya kufeli vipimo vya madawa.Lakini baada ya kuangalia uwezo wake dhidi ya Greece, unaweza kuelewa kwanini kikosi cha kuzuia matumizi ya madawa ya kulevya walienda kumgongea hodi kwenye chumba cha hotel mara tu baada ya mchezo.


8: Manuel Negrete (Mexico) vs Bulgaria, @Mexico 86

Unakumbuka hili jina? Inawezekana hukumbuki.Ingawa ni mtu anayehusika na kufunga moja ya magoli mazuri katika historia ya kombe la dunia.Kiungo huyu wa Mexico alitumia muda wake wa mwingi kucheza soka nyumbani kwao akiichezea timu ya Pumas zaidi ya michezo 400.



7: Carlos Alberto (Brazil) vs Italy, Mexico 70

Goli la nne na la mwisho kwa Brazil katika fainali ya World Cup ya kukumbukwa.


6: Roberto Baggio (Italy) vs Czechoslovakia, @iTALY 90.

Timu zote zilikuwa zimeshafuzu kwa hatua ya mtoano ya michuano hiyo, lakini taifa mwenyeji walitaka kushinda na kuwa kileleni mwa kundi, walifanikiwa na shukrani kwa goli la Roberto Baggio.


5: Archie Gemmill (Scotland) vs Holland, @Argentina 78.

Miaka 33 iliyopita “Tartan Army” walikuwa na timu ambayo ilikuwa hatari.Graeme Souness, Kenny Dalglish, Joe Jordan, John Robertson na Archie Gemmill yalikuwa majina ya wakali wa timu hiyo, na matarajio ya World Cup yalikuwa juu.Lakini baada ya kufungwa na Peru na kutoa sare na Iran, The Scots walihitaji kuwafunga Holland kwa magoli 3 ili wafuzu.Ilionekana ni vigumu na haiwezekani mpaka wakati walipokuwa mbele kwa 2-1, wakafunga goli ambalo litaishi milele katika kumbukumbu za Tartan, asante kwa Archie Gemmill.


4: Saeed Al-Owairan (Saudi Arabia) vs Belgium @USA 94

Kombe la dunia halikuwa jombe la dunia bila mtu Fulani kufanya tukio kama la huyu jamaa, kufunga goli la uwezo binafsi kama hili.


3: Dario Rodriguez (Uruguay) vs Denmark, Japan/Korea 2002

Hii listi inaonyesha kwamba wachezaji kutoka Amerika ya kusini ndio uwezo zaidi ya kufanya ya hatari dimbani, na hili la Dane lilidhihirisha vipaji walivyo watu kutoka S.A, likiwa goli la michuano hiyo.


2: Diego Maradona (Argentina) vs England, Mexico 86

Baada ya bao “Mkono wa Mungu” kulikuwa nanjia moja tu ya kuwanyamazisha mashabiki wa England, na ndipo Diego Maradona alipofunga goli bora la michuano, dakika nne baadae.



1: Dennis Bergkamp (Holland) vs Argentina, France 98

Watu wengi waliomo kwenye hii listi wametokea South America, lakini “Ice Man” ndio kinara wao akiwa anatokea barani ulaya.Halikuwa tu goli bora kiufundi pia lilikuwa ni goli muhimu sana kutofautisha na mengine kwenye hii listi.

No comments:

Post a Comment