Search This Blog

Wednesday, October 19, 2011

CHELSEA VS GENK: DE BRUYNE – NITAWAONYESHA CHELSEA WANACHOKIKOSA LEO USIKU.


Kevin De Bruyne anajipanga leo usiku kuwaonyesha Chelsea wanachokikosa kutoka kwake.

Mchezaji huyo wa Genk alikuwa kati ya moja ya wachezaji waliofuatiliwa sana na The Blues katika kipindi cha usajili kilichopita lakini ilishindikana kwenda Stamford Bridge.

De Bruyne, 20, alisema: “Nilikuwa disappointed sana wakati uhamisho wangu kwenda Chelsea ulipokwama.Nilidhani kila kitu kilikuwa kinaenda vizuri lakini haikuwa hivyo, bado nina miaka 4 katika mkataba wangu na Genk wanataka pesa nyingi kwa ajili ya uhamisho wangu.Bado naamini, labda mwakani naweza kwenda Chelsea, au timu nyingine.Sidhani kama nahitaji ku-provekila kitu katika mchezo huu mmoja.Chelsea wataniangalia hata mara 20 au 30 ili kujiridhisha.”

De Bruyne atakuwa akiangaliwa na familia yake yote at Stamford Bridge leo usiku atakapokuwa akichuana na akina Lampard.

“Kuna watu zaidi ya 12 wa familia yangu na marafiki 10 wanakuja kuniangalia nikicheza leo. Nitacheza kwa uwezo wote kuiwezesha timu kushinda na kuwafurahisha ndugu na rafiki, na mashabiki wa timu yangu.”

No comments:

Post a Comment