Search This Blog

Friday, September 23, 2011

ZANETTI NA MIAKA YAKE 16 NA INTER MILAN CHINI MAKOCHA 17

Javier Zanetti alifungua ukurasa mpya katika historia ya klabu ya Inter Milan Jumanne baada ya kuipita rekodi Giuseppe Bergomi ya michezo 756 kwa klabu hiyo ya Italia.Ingawa mafanikio ya Muargentina huyu yalifunikwa na kipigo cha 3-1 kutoka kwa Novara na kichapo ambacho kilipelekea kufukuzwa kwa kocha Gian Piero Gasperini.

Zanetti alikuwa ni moja wachezaji wa kwanza kusajiliwa kipindi Mssimo Moratti anaingia madarakani, Raisi huyo aliingia madarakani mwak 1995, miezi michache kabla Zanetti hajajiunga na Inter kutokea Banfield.

Kwa miaka 16 aliyokuwa na Inter Milan, Javier Zanetti ameichezea klabu hiyo mechi 757 chini makocha 17 na amefanikiwa kushinda makombe 16 yakiwemo matano ya Serie A, manne ya Coppa Italia, manne ya Supercoppa Italiana, moja la Champions league, UEFA Cup 1, FIFA Club World Cup 1.

No comments:

Post a Comment