Search This Blog

Thursday, September 22, 2011

Dr. Emmanuel John Nchimbi (Mb) amemteua Bw. Dionis Malinzi kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT).

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Dkt. Emmanuel John Nchimbi (Mb) amemteua Bw. Dionis Malinzi kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT).

Aidha pia amewateua wafuatao kuwa Wajumbe wa Baraza la Michezo la Taifa.

Mhe. Jenister Mhagama (Mb) Mhe.

Mkiwa A. Kimwanga (Mb)
Bw. Jamal Rwambow
Bw. Venance Mwamoto
Bw. Juma Pinto
Dkt. Cyprian Maro
Bw. Kanali Eliot Makafu
Bibi Jeniffer Mmasi
Bw. Ramadhani Dau
Bw. Alex Mgongolwa
Bw. Maulid Kitenge

Wengine ni Wajumbe wa kuteuliwa kutokana na nafasi zao:

Mkurugenzi Mkuu - Bodi ya Michezo ya Kubahatisha

Kamishna wa Elimu - Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Mwakilishi - TAMISEMI
Mkurugenzi wa Michezo – Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Mwakilishi - Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Wajumbe kutoka Wawakilishi wa Vyama vya Michezo (Makatibu) ni:

CHANETA - Chama cha Netiboli Tanzania

TPC - Tanzania Paralympic Committee
AAT - Automobile Association of Tanzania
TSA - Tanzania Swimming Association
BFT - Boxing Federation of Tanzania
RT - Riadha Tanzania
TFF - Tanzania Football Federation
TBF - Tanzania Basketball Federation
TOC - Tanzania Olympic Committee
TTTA - Tanzania Table Tennis Association

Uteuzi huu umefanywa kwa kuzingatia Mamlaka ya Waziri chini ya kifungu cha 3(2) cha nyongeza ya Katiba ya Sheria ya BMT Na. 12 ya mwaka 1967 na marekebisho yake katika Sheria Na. 6 ya mwaka 1971.

Wajumbe hao watalitumikia Baraza kwa kipindi cha miaka mitatu.



Imetolewa na Wizara ya Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo22.09.2011

1 comment:

  1. Hapa kuna mteuliwa mmoja amenishangaza ana sifa gani za kuwa mjumbe BMT. Nchi hii tunacheza na michezo. Waziri alipaswa kuwa makini zaidi.This is Tanzania, saa nyingine inashangaza sana.

    ReplyDelete