Search This Blog

Thursday, August 4, 2011

DVD yampatia nafasi ya kufanya majaribio Max Lonsdale Manchester United


Wakati Max Lonsdale alipotupiwa vilago na timu ya Macclesfield Town inayoshiriki ligi daraja la 3 nchini England msimu uliopita hakuna aliyedhani angefika hapa alipo.
Lonsdale mwenye umri wa miaka 18 alitengeneza DVD na kuipeleka kwa kocha wa Manchester Utd,Sir Alex Ferguson,
Baada ya Lonsdale kutemwa na timu yake aliamua kumtafuta Ferguson na alipompata akampatia hiyo DVD na Ferguson akampatia jukumu kocha wa timu ya wachezaji wa akiba ambaye alimpatia wiki moja ya majaribio na baadae yakawa majuma mawili.

sasa anasubiria kuona kama atapata mkataba wa kudumu.
...binafsi nimemkubali huyu dogo hakuna mafanikio yanayopatikana kwa njia nyepesi...SAFI SAANA DOGO KOMAA MPAKA KIELEWEKE..



No comments:

Post a Comment