Search This Blog

Friday, July 29, 2011

WENGER KUVUNJA REKODI YA USAJILI KWA MATA



Arsene Wenger yupo katika mipango kabambe ya kuvunja rekodi ya usajili katika klabu ya Arsenal kwa ajili ya Juan Mata huku akijipanga kuendeleza ugumu wa kumuachia Fabregas.

Wenger jana usiku alikubali kulipa ada ya £17million kwa Valencia kwa ajili ya Mata – na ameongeza ofa ya beki wa Everton Phil Jagielka kufikia £13million.

Lakini wakati Arsenal hatimaye wakijipanga kuanza kutumia katika usajili msimu huu, pia wamewapa Barcelona muda maalum wa kukamilisha uhamisho wa Cesc Fabregas.

The Gunners’ captain hatocheza katika kombe la Emirates wikiendi hii, na Arsenal wamewaambia walipe ada ya £40m au watasitisha dili hilo.

Wenger anaaminika kuweka deadline ya August 5 kupitia e-mail iliyotumwa kwenda kwa raisi wa Barca Sandro Rosell, ili mfaransa huyo apate muda wa kupanga mashambulizi ya msimu ujao.

Arsenal wamebariki uuzwaji wa Fabregas, lakini wamechoswa na kusubirishwa na Barca.

Dili la uhamisho wa Mata, 23, linawakilisha mapinduzi makubwa, baada ya ku-top kwa urahisi uhamisho wa £12m wa Andrey Arshavin in 2009.

Wenger pia ameongeza ofa nzuri kwa ajili Phil Jagielka baada ya kuona bid ya £10m ikakataliwa wiki mbili zilizopita, lakini Everton wanahitaji kiasi kisichopungua £15m.

Kama ikishindikana kumpata Jagielka, Arsenal wanaweza kurudi kwa Bolton centre-back Gary Cahil.


Kuwasili kwa Mata kunaweza kumaanisha Arshavin ataruhusiwa kuondoka, huku Galatasary wakijitokeza kumtaka, pia Sporting Lisbon wametuma ofa kwa ajili mshambuliaji Nicklas Bendtner, ingawa ofa hiyo ni pungufu kwa thamani waliyoipanga Gunners ya £12m na wareno hao wata-struggle kulipa mshahara wa £52,000.

No comments:

Post a Comment