Search This Blog

Sunday, July 24, 2011

KWA UPANDE WANGU NGASSA AMESHAFAULU MAJARIBIO YAKE- Kocha Mkuu, Sigi Schmid

Kama Mrisho Ngassa angekuwa anafanya majaribio ya kuchezea moja ya klabu za nchini kwetu Tanzania basi muda huu angekuwa tayari ameshasaini form za kujiunga na klabu hiyo,
lakini utaratibu wa kumsajili mchezaji ni tofauti kabisa kwa wenzetu,kufahamu hilo fuatilia mahojiano yangu na kocha mkuu wa SEATTLE SOUNDERS bwana SIGI SCHMID,
kifupi ni kwamba kuna hatua za kiufundi zinazofuatwa kabla ya mchezaji kusajiliwa,ni tofauti na kwetu Tanzania ambapo kiongozi mmoja huwa na nguvu na ujasili wa ajabu wa kumsajili mchezaji kwa matakwa au mapenzi yake binafsi pasipokuweka UWELEDI mbele.

haya ni mahojiano maalumu na kocha wa SOUNDERS Mr SIGI SCHMID.

UNAZUMZUNGUMZIAJE UWEZO WA MRISHO NGASSA KWA KIPINDI ULICHOKAA NAYE ?
Mrisho ngassa amenifurahisha sana,ni mchezaji aliyekamilika kwa kiasi kikubwa,anaweza kusumbua sana kutokana namna anavyocheza, kwenye mazoezi kwa siku zote amefanya vizuri na hata kwenye mechi dhidi ya Manchester Utd alifanya vile nilivyomuelekeza kufanya

NGASSA NI MCHEZAJI WA NAMNA GANI ?
kitu kingine kizuri kwa ngassa ni msikivu kila majukumu niliyompatia ameyatekeleza vilivyo, ana uwezo wa kucheza sehemu zote za pembeni,
anapenda kushambulia akitokea pembeni kushoto kwasasbabu ana mbio sana na ni rahisi kuisaidia timu pindi inapokuwa inatafuta bao,lakini pia ni mzuri akiwa anatokea kulia kwa ajili ya kusaidia pasi ili wengine wafunge,

SEHEMU GANI ANA MAPUNGUFU ?
Sijaona mapungufu sana kwani kwa namna anavyotakiwa kutumika amekamilika lakini cha ziada ni kuongeza nguvu kidogo tu ili aweze kushindana pasipokuwa na wasiwasi kwenye MLS (MAJOR LEAGUE SOCCER )

NINI NAFASI YAKE Font sizeKWENYE KIKOSI CHAKO CHA SOUNDERS KWA SIKU ZA BAADAE?
Kwa upande wangu hakuna tatizo hata kidogo,kifupi nimemkubali ila kuna watu wengi sana wanaoamua mchezaji kusajiliwa, general manager ana mkono wake,chief scout naye ana mkono wake na pia kama ulivyooona kuna wasaidizi wangu wengi kwenye benchi la ufundi,kila mmoja ana jukumu lake kwahiyo nasubilia ripoti zao alafu nikae na wakurugenzi na viongozi wengine ili uwamuzi wa pamoja utolewe.

RIPOTI YAKO BINAFSI INASEMAJE KUMUHUSU NGASSA
Kama nilivyokwambia awali kwangu hana pingamizi. Tatizo ni kwenye management, wao ndiyo wanaojua yupo hapa kwa muda gani, kama maamuzi yangekuwa yangu pekee basi huyu mchezaji asingeondoka tena hapa.

hapa ilikuwa ni baada ya mazoezi ya leo kocha Sigi Schmid (kushoto ) akiteta jambo na mmiliki na General manager wa SOUNDERS Mr Adrian Hanauer ( mwenye pensi ya khakhi )


kocha mkuu wa SEATTLE SOUNDERS Mr SIGI SCHMID akiwa na MRISHO NGASSA mara baada ya mazoezi ya leo.






hapa ilikuwa baada ya kumaliza kufanya mahojiano yetu,pia haya mahojiano utayapata kupitia SPORTS XTRA ya CLOUDS FM.






NGASSA mara baada ya mazoezi ya leo akiwa na kiungoAMADOU toka nchini Gambia.ambaye pia wanaishi nyumba moja.












JAMANI! JAMANI! hili ni benchi la ufundi la SOUNDERS kila mmoja wao hapa ana jukumu lake, waangalie kila mmoja alivyokuwa makini akifuatilia NG'ADO KWA NG'ADO ( kwa ukaribu mno ) kila kinachoendelewa wakati wa mazoezi..














No comments:

Post a Comment