Search This Blog

Sunday, July 24, 2011

COPA AMERICA FINAL: PARAGUAY VS URUGUAY-LARISSA KUTIMIZA AHADI YAKE

Michuano ya kombe la mataifa ya marekani ya kusini Copa America inafika tamati kwa mchezo wa fainali kati ya Paraguay na Uruguay. Ni fainali ambayo hakika itakuwa na mvuto kwa kuwa kila timu hizi zinapokutana kuna uhakika wa magoli si pungufu ya matatu na kuna kila sababu ya takwimu hii kuendelea . Ukitazama Historia ya Copa America kama inawapendelea Uruguay kwa kuwa wametwaa Copa America mara 14 na wanatafuta kuweka rekodi ya kutwaa kombe hili kwa mara ya 15. Katika michezo michache waliyocheza Uruguay na Paraguay kwenye Copa America Paraguay wameibuka na ushindi mara nne na hiyo pekee inatosha kuwapa waparaguay sababu ya kushinda japo hadi fainali hawajaweza kushinda mchezo hata mmoja wakitoka sare mara zote wanazotia timu .

Paraguay wanaweza kuwa na sababu ya ziada ya kufanya vizuri kwenye mchezo huu nayo ni jina la mwanamitindo Larissa Riquelme. Mrembo huyu alileta balaa kwenye kombe la dunia nchini ‘ssauzi’ kwa nadhiri aliyoiweka ambayo iliwafanya mashabiki wengi waiombee Paraguay itwae kombe la dunia ili mradi tu waweze kumshuhudia mrembi huyu akitimiza nadhiri aliyoiweka . Larissa aliapa kuwa ikiwa Paraguay itatwaa kombe la dunia atasaula nguo zake zote katikati ya uwanja na kushangilia na wachezaji wa timu yake ya taiafa na akasema atarudia kufanya hivyo mitaani nchini kwao Paraguay . Bahati mbaya kwa watu walioomba Paraguay ishinde kwani haikuwa hivyo na hawakuweza kuona vimbwanga vya mrembo Larissa .

Maombi ya wato wote waliotaka kumshuhudia Larissa akitimiza nadhiri yake yanaonekana kutimia kwani Paraguay wamefuzu kucheza fainali ya kombe la mataifa ya marekani ya kusini ambapo wanakutana na Uruguay . Larissa Riquelme amerudia tena azma yake na amesema kuwa ikiwa Paraguay itashinda dhidi ya Uruguay basi atasaula nguo zake zote ana ataungana na wachezaji wa Paraguay uwanjani kushangilia na pia atarudia hayo tena nyumbani kwa Paraguay mitaani ambapo ataonyesha furaha yake kwa Paraguay kupata ushindi .Tungoje kuona kama tutapata bahati ya kushuhudia mrembo huyu aliyechizika na mchezo wa soka akitimza nadhiri aliyoiweka , kazi kwenu kina Lucas Barios , Roque Santa Cruz , Nelson Haedo Valdez na Justo Villar ,mpeni raha mwanadada Larissa Riquelme.

No comments:

Post a Comment