Search This Blog

Tuesday, April 8, 2014

UCL ROBO FAINALI: TAKWIMU - CHELSEA WENYE REKODI NZURI NYUMBANI VS PSG HATARI ZAIDI UGENINI - MADRID HATA WAKIFUNGWA 4-1 TENA WATAPITA


Chelsea FC (1) v Paris Saint-Germain (3)
• Chelsea wameruhusu wavu wao kuguswa katika mechi moja tu kati ya tano walizocheza Stamford Bridge dhidi ya timu kutoka Ufaransa lakini PSG wamefunga mabao 14 katika mechi nne za ugenini msimu huu katika mashindano haya na wameshinda mechi zao 6 za mwisho kati ya 11 za UEFA Champions League, wamepoteza mechi 2 tu. 
• The Blues wameshinda mechi 7 kati ya 12 za mashindano ya UEFA ambapo mchezo wa kwanza wanakuwa wamefungwa. Waliwatoa SSC Napoli kwa 4-1 baada ya muda wa ziada katika 2011/12 UEFA Champions League raundi ya 16  – walifungwa 3-1 ugenini - walishinda mechi hiyo na kwenda mpaka kutwaa ubingwa. 
   

Borussia Dortmund (0) v Real Madrid CF (3)
• Ushindi wa Madrid wa 3-0 katika uwanja wa Santiago Bernabéu unamaanisha kwamba wanaweza kuruhusu kufungwa tena 4-1 kama msimu uliopita katika nusu fainali na bado watapita. 
• Madrid wamefunga katika mechi zote za ugenini (22) katika UEFA Champions League tangu walipofungwa 1-0 na Olympique Lyonnais katika hatua ya 16 bora ya msimu wa 2009/10, walitolewa 2-1 on aggregate. Madrid wamefungwa mara nne - mara 3 kati hizo nchini Ujerumani - katika mechi zao 22 za mwisho walizocheza ugenini kwenye mashindano haya. 

No comments:

Post a Comment