Search This Blog

Wednesday, April 2, 2014

MAKALA: MISHAHARA NA UWAJIBIKAJI NI TATIZO KWA YANGA SC?


Na Baraka Mbolembole

Majuzi nilizungumza na mchezaji mmoja wa timu ya Yanga SC. Ni rafiki yangu wa miaka mingi sana toka tukiwa mkoani tukicheza soka pamoja.
Tulikuwa tunazungumzia kuhusu kiwango chake cha sasa, na nilimwambia amekuwa bora na si rahisi kwake kurudi katika benchi. 
Kama ilivyo wachezaji wengine wengi, naye alishukuru ila akaniambia ' Nimeshika kwa muda nafasi ya Mtu'.Nilipingana naye kuhusu hilo nikamwambia 'Huu ni wakati wako, utakuwa mchezaji wa kutegemewa wa timu ya Taifa si muda kuanzia sasa'.
Namfahamu vizuri! Ni mchezaji mwenye nidhamu ndani na nje ya uwanja. Anaupenda mpira. Mpambanaji. Mtu jasiri, na mchezaji mwenye maarifa mengi ndani ya uwanja.

Nilimkumbusha kila kitu, tangu akianza kucheza ligi kuu na kufunga mabao nane katika msimu wake wa kwanza akicheza kama mlinzi wa kulia katika timu iliyo daraja la chini kwa sasa. Nikwambia, ' Wewe jiamini tu, nafikiri umeandaliwa kuwa mrithi wake. 
Sasa timu zinafungwa katika kusaini wachezaji wengi kutoka nje ya nchi, hivyo watahitaji kuona wachezaji wazawa kama wewe ambao tayari mmekomaa mnabaki kuwa msingi wa timu.

Ndiyo wakati fulani wachezaji wazawa wanaona hawana nafasi ya
kupambana na kushinda vita ya kuwania namba dhidi ya wachezaji kutoka nje ambao usajiliwa na kulipwa pesa nyingi kuliko wao. Lakini bado tumeweza kuona kocha wa Yanga, Hans alipanga wachezaji wazawa nane kati ya 11 katika kikosi kilichoanza mechezo dhidi ya Azam, Emmanuel Okwi, Didier Kavumbagu, na Hamis Kizza walikuwa wachezaji pekee kutoka nje na wote walianza katika safu ya mashambulizi.

Je, kukosekana kwa Mbuyu Twite kulikuwa tatizo kwa Yanga?. Mbuyu ana uwezo wake!, ni mchezaji mzuri kutoka nje ya nchi ambaye timu yake inajivunia kuwa naye. Lakini bado tunaona mbadala wake akimudu jukumu la beki namba mbili. Ni hivyo hivyo kwa Haruna Niyonzima. 
Ni kiungo wa aina yake ambaye anaweza kuleta tofauti ya mchezo muda wowote kutokana na uwezo wake wa kupiga mashuti ' on target', pasi za mwisho, mmiliki wa eneo la katikati ya uwanja. Yanga walimmiss sana Niyonzima katika mchezo dhidi ya Azam, na Mnyarwanda huyo ndiye aliyeleta tofauti katika mechi baina ya timu hizo msimu uliopita kwa kufunga bao kali la umbali akiwa katika 'pembe ya uwanja'.

Lakini kuanzia mchezo wa marejeano dhidi ya Al Ahly, Yanga wameona wanaweza kusonga mbele bila Haruna. Wachezaji mbada wamekuwa wakicheza kwa kujituma, ila wamekosa matokeo katika siku za karibuni. 
Mazungumzo yangu na mchezaji huyo ndiyo yaliyonifanya niandike makala hii. Kwani wakati nikimweleza umuhimu wake na nafasi anayocheza kwa sasa ni lazima atatesa. Akanishtua kwa kuniambia jambo ambalo linabeba kichwa cha habari cha hoja yangu ya leo.

MISHAHARA NA UWAJIBIKAJI NI TATIZO KWA YANGA?
, Imekaa katika muundo wa swali kwa kuwa ni hoja inayofungua milango kwa mtu mwingine kutoa mawazo yake. Pamoja na umuhimu wote ambao amekuwa akionesha katika kikosi, bado mchezaji huyo aliniambia. 
 Hawa jamaa ( Yanga) hawaeleweki' ni kamuuliza kwa nini anasema hivyo. ' Unajua sisi wanatuona watoto. Tunafanya kazi kubwa uwanjani lakini wenzetu ndiyo wamekuwa wakilipwa pesa nyingi'

Nikamwambia, hapana! Hiyo siyo sababu ya kumfanya alalamike. Yeye aendelee kufanya kazi yake vizuri uwanjani kama anavyofanya sasa, mwisho kiwango chake ndicho kinapandisha thamani ya malipo yake.
Nikamwambia kila mchezaji nyota duniani alianza kulipwa '
kidogokidogo' na viwango vyao ndiyo vilipandisha thamani yao.
Akaniambia, ' Sawa, lakini huu ni wakati ambao na mimi natakiwa kuvuna kinachonikidhi. Nina familia, na watu wanaonitazama. Mimi siyo mtoto tena'

Nilipojaribu kumdadisi kama kuna tatizo lolote kati yake na timu,
akaniambia hakuna.nafikiri mchezaji huyu anatakiwa kusikilizwa kwa umakini mkubwa na viongozi wa Yanga. Kwa nafasi yake itawachukua muda kumpata mchezaji kama yeye, bado ni kijana na tayari yupo hapo kwa msimu wa tatu sasa. 
Kama walianzisha kikosi cha wachezaji nane katika mchezo muhimu dhidi ya Azam, huku kundi kubwa la wazawa hao wakiwa ni vijana, kumsaini tena Omega Seme kwa dau la millioni 20, hiyo ni ishara kuwa ' Yanga yenye sura ya Kitanzania zaidi itaonekana msimu ujao' lakini inakuwaje kushindwa kumsaini mchezaji wa nafasi muhimu kama mlinzi wa pembeni kwa sababu za mshahara?

'Mkataba wangu unamalizika mara baada ya msimu huu kufika mwisho. Nimewambia wanipandishie malipo lakini wamekuwa wazito, ni kama hawapo tayari kwa jambo hilo.' Hapana pia pana pointi zake pia. Mkataba unapokwisha inatakiwa kutazamwa mchango na uwajibikaji wa muhusika.
Kama alikidhi viwango, anatakiwa kupewa mkataba ulio bora zaidi, kama anahitajika katika malengo yajayo ya klabu ni muhimu kumuhifadhi mchezaji huyo. Yanga wamesaini wachezaji wengi kutoka ng'ambo na wanalipwa vizuri lakini kilio cha mchezaji huyu kinamaanisha kuwa kuna kundi la wachezaji wengi wanaocheza mara kwa mara linalipwa kiwango
cha chini cha mishahara. Kuna tofauti kubwa katika mishahara ya
wachezaji kama Okwi, Mbuyu, Haruna, Kiiza na Kavumbagu na wachezaji wazawa.

Lakini unapofika wakati wazawa hao wanapoomba walau ongezeko kidogo ya mishahara hufungiwa vioo, wale ambao bila kucheza Yanga hawawezi kuwa wachezaji wazuri, wamekuwa wakisaini mikataba mipya kwa mishahara 'kiduchu'. 
Ndiyo kuna wakati bora kuchukua kilichopo kuliko kukosa
kabisa. Ila, mbeleni inaweza kuwa tatizo kwa klabu endapo wazawa hao
watajikuta wapo wengi. Je, ni kiasi gani mchezaji huyo anahitaji ili
kubaki Yanga na kusaini mkataba mpya?

Sikumuuliza kiwango halisi anachotaka ila nilimuomba aniambie kwa makadirio ni kiasi gani anataka walau Yanga wafikie kama mshahara wake, Mil. 1.5, itatosha. Huu si wakati wa kucheza soka kwa mapenzi.
Mimi nimesimamia hilo la nyongeza yangu ya mshahara, nitasaini
wakifikia lakini ni kama hawataki. Nitaondoka msimu ukimalizika endapo watashindwa kufikia mshahara huo, Tunajituma sana, ila wapo wachezaji wengine wanalipwa zaidi japo hawana mchango mkubwa. 
Yanga imeporomoko kutoka nafasi ya kwanza hadi ya pili katika msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara.

Wapo nyuma kwa tofauti ya pointi saba dhidi ya Azam Fc, na watacheza na JKT Ruvu siku ya jumapili hii katika uwanja wa Taifa. Wakati, Azam watakuwa ugenini kucheza na Ruvu Shooting, mjini Mlandizi. 
Je tofauti kubwa ya mishahara ni tatizo kwa Yanga wakati huu hasa wachezaji wakitoa malalamiko kuwa kuna upendeleo fulani unaofanywa na viongozi kwa baadhi ya wachezaji?., Wachezaji nafikiri wanapopandisha viwango vyao wanatakiwa kulipwa vizuri. Ndivyo inavyotokea hata katika dunia ya kina Wayne Rooney, Cristiano Ronaldo, Leonel Messi, mikataba mpya inakwenda na thamamini ya mchango wa mchezaji katika mkataba uliopita.
Mchezaji huyu asikilizwe Yanga.
0714 08 43 08

9 comments:

  1. Huu ni mwendelezo wa makala za kutaka kuivuruga yanga kisaikolojia zilizoanzishwa tangu ilipofungwa na Mgambo.Ukweli ni kwamba kila mchezaji thamani yake hupimwa wakati wa kusaini mkataba na asipojithaminisha vizuri hayo ndiyo matunda yake.Haiwezekani wachezaji wote wawe na mshahara unaolingana kwa sababu mshahara huamuliwa wakati wa majadiliano ya mkataba na baada ya hapo kuna kiwango kupanda,kubaki kilivyo au kushuka lakini mshahara hubaki palepale hadi mwisho wa mkataba

    ReplyDelete
  2. Hivi kwa nini kwa nini Yanga ni watu wa kulia lia tu, wa kuhusi hujuma hujuma tu, wakati ni ukweli kwamba wao ndiyo wanaongoza kwa kuihujumu Simba kwa njia mbali mbali. Au mtenda akitendewa anahisi kaonewa saaana.

    Maana sasa Yanga watagombana na wana blog wote wa Bongo, walianza kwa Bin Zubeiry sasa wanahamia huku.

    ReplyDelete
  3. Mimi si shabiki na wala siipendi yanga kabisaaa lakini najaribu kutafuta mantiki ya makala yako siipati, kwa ufupi sio mawazo ya kujenga nshahara unapandishwa kwa taratibu zake sio kwa maneno yako ya kichochezi

    ReplyDelete
  4. Mantiki yako ni ipi katika hilo??unampigia debe mchezaji au la!!Weka uchambuzi yakinifu..Unataka kuniambia kati ya Hazard na Lampard nani anafanya kazi kubwa uwanjani na nani analipwa hela nyingi!!Yaani bongo bwana kila kitu siasa!!Wakati mwingine Kama hamna mada kaeni kimya!!Sio mnatuletea story ambazo hazina kichwa wala miguu..Hivi unajua maana ya mkataba?Huo ni uchambuzi kanjanja..Wakati mwingine sio lazima wote tuwe wachambuzi..Mnaandikaandika tu..Hivi unajua Januzaji baada ya kuongezewa mkataba malipo yake bado ni madogo kuliko wachezaji wa man u wanaokaa bench!!Unajua Torres analipwa sh.ngap?je mchango wake uwanjani ukoje?Nenda kajifunze kuhusu mikataba ya wachezaji sio mnaandikaandika tu..

    ReplyDelete
  5. Kwanza umekosa umakini kwenye makala yako unazungumzia mchezaji aongezwe mshahara kwa performance ya mechi mbili makala yako imejaa ushabiki na mahaba kwa huyo mchezaji uliyecheza nae mkoani.

    ReplyDelete
  6. Huyo mbumbumbu aliyecomment namba 2 hapo juu nafikiri ukiwapanga mashabiki wa wote mbumbumbu sc ukawapa mtihani yeye atakuwa wa mwisho,

    ReplyDelete
  7. Tuliwahi kuzungumza hapa kuwa kuna watu wanatumiwa kwa ajili ya watu Fulani dhahiri inaonekana..baraka unarudia tena kutumiwa au kama hutumiwi basi Una matatizo makubwa sn kichwani mwako..inawezeka hata taratibu za ajira huzijui kwa kuwa hukuwahi kupata kuajiriwa hapo kabla!inashangaza sn kwako kushindwa kutofautisha posho na mshahara..wacha tukusaidie uelewe..mshahara ni siri kati ya muajiri na muajiriwa..mshahara ni makubaliano ya muajiri na muajiriwa na wote wawili hawa wanatambua kuwa ni siri na haipaswi kutoka kwa mtu mwingine..kwa maana hiyo we ulikaa na mchezaji uliemtaja akakueleza siri ambayo hakutakiwa akueleze!kama ni kweli basi mchezaji huyo hafai kubaki katika timu na kwa jinsi ulivyokuwa umemuweka hadharani tumemjua kuwa ni juma Abdul!!..ndio aliempokea mbuyi twite juzi kati hapa jamani..kama juma kwa kiwango anachokionesha ss kwa mechi 3 alizocheza huku ya Azam akishindwa kumkaba John boko mpk akatoa pasi kwa sureboy iliyosababisha bao la kusawazisha,kiwango chake bado sana na ndo maana kakwambia bado hana namba ya uhakika ya kudumu..ataendeleabsn kusubiri kama twite atakuwepo bado yanga..huu ni uchochezi mwingine..hatutokaa kimya kuona jambo Fulani linapotoshwa kijinga halafu tunaangalia tu,ntakukosoa kila utakapokuwa unataka kutuaminisha ujinga Wako..we umri huo ushindwe kutofautisha posho na mshahara!,kweli utaandika kitu cha kunifanya mtu mwenye uelewa wngu nikuone mbumbuu na mbulula tu

    ReplyDelete
  8. Mbumbu ni wewe uliye comment namba sita, timu gani hii ikifungwa ni hujuma hujuma, hujuma tu. Basi ligi ilivyoanza mngepewa point zote tatu kwa kila mechi bila ya kuingia uwanjani. Zinafungwa barcelona, bayern munich sembuse Ndala za Jangwani. Jadili mada iliyopo, siyo kuanza personal attack, hujuma hujuma, mnataka hawa wanablog wawashikie miguu mfunge. Mara maandamano timu ya mpira na maandamano wapi na wapi? Mara Bahanuz kahujumu Misri, angalieni wanaojua mpira walivyowafungasha virago Al Ahly ya Misri Mabingwa wachovu. Haya leo Kaseja, Yondani, Chuji wamefungisha Mgambo. Wapelekeni basi TAKUKURU waliotoa na kupokea wafungiwe maisha. Umbumbu wenu wa mpira ndiyo unaoua Soka Tanzania kwa pesa zenu za kifisadi. Waacheni watu wa mpira waoneshe njia. Hata Jamal ameshawachoka. Azam wana wachezaji wengi wa Academy, wametoa wachezaji wengi timu ya taifa vijana, mechi yao na Ruvu imehairishwa mnadai hujuma hujuma. Vya kulea hamuwezi mmezoea vya kunyonga kwa pesa zenu za kifisadi. Subirini sasa Rungu litakaloshuka toka FIFA kwa Okwi, sijui mtaandamana mpaka FIFA? Sababu mmezoea kuhonga, mkifungwa mnafikiri mmezidiwa kete kwenye mchezo wenu huo huo, ndio maana wachezaji wenu hawana nidhamu ya mazoezi, wanashinda vilabu vya usiku kabla ya mechi, wameoa wake watatu, my foot eti ndiyo maprofeshno wa Kandambili.

    ReplyDelete
  9. Siku zijazo naomba mwenye hii blog awalazimishe wachangiaji kuweka na CV zao ili asichanganye kwa pamoja wenye akili timamu na mbumbumbu ambao hawakawii kwenda kung'oa viti na kuvunja milango uwanja wa Taifa.

    ReplyDelete