Search This Blog

Wednesday, March 26, 2014

PEP GUARDIOLA AIONGOZA BAYERN KUTWAA UBINGWA WA HARAKA ZAIDI KATIKA HISTORIA YA BUNDESLIGA


History iliandikwa jana usiku! FC Bayern München wamefanikiwa kutwaa ubingwa wa 23 wa Bundesliga baada ya michezo 27 tu - huu ndio ubingwa wa haraka zaidi katika historia ya Bundesliga.

Ubingwa huu ni wa tatu kwa Pep Guardiola katika msimu wake wa kwanza, alishinda UEFA Super Cup mwaka jana mwezi August, kisha wakashinda ubingwa wa klabu bingwa ya dunia December mwaka jana.

Je Guardiola ataweka rekodi ya kubeba makombe manne ndani ya msimu wake wa kwanza na Bayern Munich kwa kuchukua ubingwa wa klabu bingwa ya ulaya?

No comments:

Post a Comment