Search This Blog

Friday, March 7, 2014

OKWI NA KIIZA TAYARI WAMETUA NCHINI MISRI!

 Washambuliaji wa Yanga, Emmanuel Okwi na Hamis Kiiza wamewasili jijini Cairo usiku wa manane wakitokea nchini Zambia walikokuwa na timu ya Taifa ya Uganda tayari kuwakabili Al Ahly hapo siku ya jumapili mjini Alexandria.
Wachezaji hao walipokelewa uwanja wa ndege wa Cairo na afisa habari wa timu hiyo Baraka Kizuguto pamoja na maafisa wawili kutoka ubalozi wa Tanzania nchini Misri.
         Kiiza,Okwi na Shaffih mara baada ya kufika uwanja wa ndege wa Cairo.

Mara baada ya kuwasili wachezaji hao walielekea moja kwa moja kwenye kambi ya timu iliyopo nje kidogo ya mji wa Cairo.


No comments:

Post a Comment