Search This Blog

Wednesday, March 12, 2014

FC BARCELONA VS MANCHESTER CITY - TIMU YA MWISHO YA ENGLAND KUIFUNGA BARCELONA CAMP NOU ILIKUWA LIVERPOOL - CITY WATAWEZA LEO?



Barcelona wamepoteza mchezo mmoja tu kati ya 18 ya mwisho waliyocheza katika hatua ya mtoano ndani ya dimba la Camp Nou kwenye michuano ya Champions League (0-3 v Bayern Munich msimu uliopita).

Kati ya michezo 30 ya hatua ya mtoano ya michuano ya Champions League iliyopigwa Nou Camp, Barcelona wamepoteza michezo miwili tu kwa angalau mabao yasiyopungua mawili (0-2 v Real Madrid in April 2002 na 0-3 v Bayern Munich in May 2013).

Ni klabu moja tu ya kiingereza iliyoweza kufanikiwa kuifunga Barcelona katika dimba la Camp Nou kwenye Champions League (kwenye michezo 17): Liverpool mnamo February 2007 (1-2).

Mechi 3 za mwisho za Champions League kati ya Barca dhidi ya timu za England ndani ya dimba la Camp Nou zimezalisha mabao 13.

Manchester City hawajawahi kushinda dhidi ya klabu ya Uhispania kwenye michuano ya Champions League.

Manchester City wameshinda mechi zao tatu za ugenini kwenye Champions League msimu huu, ukiwemo ushindi wa 3-2 dhidi ya mabingwa watetezi Bayern Munich.

Manchester City wameweza kuzuia wavu wao kuguswa mara moja katika mechi 13 za mwisho za Champions League (ushindi wa 3-0 dhidi ya Viktoria Plzen)

Barcelona ndio timu yenye rekodi nzuri zaidi ya kufunga katika uwanja wa nyumbani kwenye michuano ya Champions League msimu wakiwa wameshafunga mabao 13.

Barcelona wamefanikiwa kufika nusu fainali ya ligi ya mabingwa ya ulaya mara sita mfululizo, rekodi bora kabisa katika michuano hii.

Lionel Messi (mabao 66) amebakiza mabao matano 5 tu kufikia rekodi ya mabao Raul ya kufunga mabao mengi katika Champions League (mabao 71). Amefunga mabao 7 katika mechi 4 msimu huu - akiwa kapiga mashuti 9 tu langoni.

Xavi ameshaichezea Barcelona mechi 138 katika Champions League. Ikiwa atacheza leo ataifikia rekodi ya kucheza mechi nyingi katika michuano hii inayoshikiliwa na Ryan Giggs aliyecheza 139.

No comments:

Post a Comment