Search This Blog

Thursday, March 13, 2014

ERIC CANTONA ARIPOTIWA KUKAMATWA KWA KUMSHAMBULIA MTU LONDON

Mchezaji wa zamani wa Manchester United Eric Cantona amekatwa jijini London akituhumiwa kufanya shambulio la mwili. 
Mwanasoka huyo wa zamani wa Ufaransa ambaye aligeukia uigizaji wa filamu alikamatwa na polisi kuafuatia ripoti aligombana na na mwanaume mwingine. 
Polisi waliitwa kwenye eneo la tukio Primrose Hill kufuatia ugomvi uliotokea wakati wa chakula cha mchana jana jumatano. 
Msemaji wa polisi wa Metropolitan: “Tuliitwa kwenye eneo la tukio 12.55pm kufuatia ripoti ya shambulio. Maofisa wa polisi walifika eneo la tukio na kumkamata mwanaume mmoja mwenye miaka 40."
Mashabiki kadhaa kupitia Twitter waliripoti kwamba walimuona Cantona jana katika kituo cha polisi huko Primrose Hill.
Cantona, 47, aliichezea United kwa miaka sita 1990s, akiifungia timu hiyo mabao 64.

No comments:

Post a Comment