Search This Blog

Friday, March 14, 2014

BODI YA LIGI NA TFF NDANI YA BIFU ZITO: NI BAADA YA BODI HIYO KUKATAA KUFANYIWA UKAGUZI WA MATUMIZI YAO YA FEDHA.

Taarifa za uhakika ambazo mtandao huu umezipata ni kwamba kuna hali ya kutoelewana kati ya TFF na bodi ya ligi.

Chanzo cha kutokuwepo kwa maelewano mazuri baina ya uongozi wa bodi na TFF ni kutokana na viongozi wa bodi ya ligi kukataa kukaguliwa mahesabu ya matumizi yao ya fedha.

Inasemekana kwamba uongozi wa Jamal Malinzi ulivyoingia madarakani uliwasaliana na bodi ya ligi ukiwaeleza kwamba ungewatumia mkaguzi wa mahesabu bodi ya ligi kwa ajili ya kukagua matumizi yao.

Lakini katika hali ya kushangaza bila sababu ya msingi na yenye mashiko uongozi wa bodi ya ligi ulikataa kumpokea mkaguzi wa mahesabu, hali iliyopelekea kutokuelewana baina ya TFF na bodi hiyo.

No comments:

Post a Comment