Search This Blog

Friday, March 7, 2014

BARUA YA WAZI YA DAVID MOYES KWENDA MASHABIKI WA MANCHESTER UNITED

Kocha wa Manchester United David Moyes ameandika barua ya wazi kwa mashabiki wa klabu hiyo akielezea kwamba msimu wake wa kwanza ndani ya klabu umekuwa m'bovu zaidi kuliko ilivyotegemewa.

Akiwasifu mashabiki kwa uvumilivu wao, Mscotish ambaye aliteuliwa na Sir Alex Ferguson, amekiri kwamba matokeo yao mabovu yamemshangaza mpaka yeye lakini ana uhakika kila kitu kitakaa sawa mbeleni.

"Wakati nilifahamu hii kazi ingekuwa na changamoto nyingi wakati nilipopewa jukumu hili, lakini msimu mgumu tulionao hakikuwa kitu ambacho nilikifiria, jambo ambalo nina uhakika mashabiki wote hawakudhani hali ingekuwa hivi," aliandika Moyes.

"Wachezaji wangu, na makocha wenzangu wanajaribu kwa kila kuhakikisha timu inarudi katika kufanya vizuri.

"Wote tumezoea kuiona Manchester United inayofanikiwa na sapoti mliyowapa wachezaji na mimi katika kipindi chote cha msimu ni kubwa sana. Tunapocheza ugenini mashabiki wetu waliosafiri wameendelea kuwa bora kabisa katika nchi hii na wakati tunapokuwa Old Trafford imani yenu kwenye timu imekuwa ikionekana wazi.

"Kuisapoti timu yenu wakati inashinda ni rahisi lakini ni ngumu sana wakati mambo yanapokuwa yanaenda vibaya, nyinyi mmekuwa nasi katika kipindi chote."

 "Kila magumu tunayopitia yatatufanya tuwe bora zaidi, timu imara na klabu bora huko mbeleni.

"Kwa miaka mingi sasa mmekuwa mkishuhudia vikosi vya ushindi na kwa muda fulani, nina uhakika kabisa tutaiona Manchester United tuliizoea."

No comments:

Post a Comment