Search This Blog

Tuesday, February 25, 2014

PREVIEW: BORUSSIA DORTMUND VS FC ZENIT - WARUSI WANATAKA KUANDIKA HISTORIA DHIDI YA KIBOKO YA REAL MADRID

FC Zenit wana nafasi ya "kuandika ukurasa mpya kwenye kitabu cha historia" na kuweka rekodi ya kufika kwenye robo fainali ya UEFA Champions League. Haya ndio maneno kocha Luciano Spalletti aliwaambia wachezaji wake wakiwa wanajiandaa na mchezo dhidi ya Borussia Dortmund ikiwa ni mara ya pili kwa klabu hiyo kucheza kwenye hatua hii. Walifungwa na Benfica katika hatua hii miaka miwili iliyopita.


Matokeo ya timu zote katika mechi za ligi wikiendi iliyopita.
• Zenit hawajacheza mechi za ligi tangu december 6, 2013 walipotoka sare na FC Lokomotiv Moskva katika Premier-Liga. Wamecheza mechi za kirafiki nchini Qatar, Israel na Turkey, walimaliza raundi ya mechi za matayarisho katika suluhu dhidi ya mabingwa wa Belarus FC BATE Borisov tarehe 16 February. Watacheza tena kwenye ligi mnamo 9 March nyumbani dhidi ya FC Tom Tomsk.
Bundesiliga: Hamburger SV 3-0 Borussia Dortmund (Jiráček 42, Lasogga 58, Hakan Çalhanoğlu 90+1)
Weidenfeller; Piszczek, Friedrich, Sokratis, Schmelzer; Bender (Reus 46), Şahin; Aubameyang, Mkhitaryan, Grosskreutz (Hofmann 75); Lewandowski (Ducksch 67).
Hamburg, ambao walikuwa wamefungwa mechi zao 8 za nyuma katika mashindano yote, waliimaliza Dortmund katika kipigo chao kizito cha msimu. 
Habari za timu
Danny na Cristian Ansaldi watakuwa nje baada ya kupata majeruhi katika mchezo wa kirafiki dhidi ya BATE.  Roman Shirokov anaendelea vizuri na matibabu ya kisigino hata hivyo ataukosa mchezo dhidi ya Dortmund. 
Marco Reus na Sven Bender ambao walikuwa na majeruhi walirudi dimbani wikiendi iliyopita baada ya kukaa nje kwa wiki mbili, lakini Bender anaweza kukaa nje mpaka May baada ya kupata majeruhi tena katika mchezo wa jumamosi. Hummels anaweza kucheza, wakati Erik Durm ana tatizo la paja. İlkay Gündoğan (mgongo), Neven Subotić (goti) na Jakob Błaszczykowski (goti) wote hawatakuwepo.
TAKWIMU
• Hii ni mara ya pili kwa klabu hii ya Urusi kuweza kupenya mpaka kwenye hatua ya 16 bora. Msimu wa  2011/12 waliifunga Benfica 3-2 nyumbani, Roman Shirokov alifunga mara mbili, lakini wakaenda kufungwa 2-0 ugenini na kutolewa. 

No comments:

Post a Comment