Search This Blog

Tuesday, January 7, 2014

SEMINA YA WAAMUZI, MAKAMISHNA JAN 13

Semina ya waamuzi na makamishna wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inafanyika Januari 13 na 14 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ndiye anayetarajiwa kufungua semina hiyo.

Wakati huo huo, Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) kimemwalika Rais Malinzi kuwa mgeni rasmi kwenye mechi ya robo fainali ya Kombe la Mapinduzi kati ya Simba na Chuoni itakayochezwa kesho (Januari 8 mwaka huu) saa 2 usiku Uwanja wa Amaan.

No comments:

Post a Comment