Search This Blog

Thursday, January 23, 2014

KUUMIA KWA FALCAO NI PIGO KWA COLOMBIA & KOMBE LA DUNIA.



Habari mbaya leo kwenye michezo ni kuhusu majeraha ya mshambuliaji  Radamel Falcao aliyoyapata jana usiku kwenye mchezo kati ya timu yake ya Monaco dhidi ya timu ya ligi daraja la nne ya Chasselay kwenye kombe la Ufaransa.

Kwenye mchezo huo Falcao alifungia bao la kuongoza wakati timu yake ya Monaco ilipopata ushindi wa mabao 3-0 kabla ya kuumia, taarifa zilizotoka leo baada ya vipimo zinasema jeraha hilo litamuweka nje kwa kipindi cha miezi sita na kupelekea kuzikosa  fainali za kombe la dunia baadae mwezi wa sita nchini Brazil.

Kukosekana kwa Falcao kwenye mashindano hayo sit u pigo kwa nchi yake ya Colomboa bali litakuwa pigo kwa mashindano hayo kumkosa mshambuliaji huyo.

No comments:

Post a Comment