Search This Blog

Friday, January 17, 2014

KUONA SIMBA VS MTIBWA SH.5000


MABINGWA wa michuano ya mtani Jembe, timu ya Simba,
kesho inashuka katika Uwanja wa Taifa kuvaana na timu ya
Mtibwa Sugar, huku kiingilio cha chini kikiwa sh.5000.
Mchezo huo utakaoanza saa 10 jioni, ukiwa wa kirafiki,
kwa ajili ya kuziweka timu hizo sawa kabla ya kuanza kwa
Ligi Kuu tanzania Bara, inayoanza kutimua vumbi wiki
ijayo.



Simba inaingia dimbani ikiwa inatoka kwenye mashindano
ya Mapinduzi, ambapo Simba ilichukua ushindi wa pili.
Katika mchezo huo Simba iliyopo chini ya kocha Zdravko
Logarusic akisaidiana na Suleiman Matola, imepanga
kutumia wachezaji wake, wote ili kiwe kipimo tosha kabla
ya Ligi Kuu.
Timu hiyo inayoshika nafasi ya nne katika msimamo wa
Ligi, imejipanga kuhakikisha inavuka mpaka nafasi ya
kwanza huku kocha wao Logarusic, akisema ana uhakika
kikosi chake kitaibuka na ushindi.



Logarusic, alisema kuwa mchezo huo ni moja ya mtihani
wake wa kutambua kikosi chake, kabla ya kuanza kwa ligi
kuu.
Alisema ameambiwa kuwa Mtibwa Sugar, ni moja ya timu
nzuri hivyo anajua kwake ni kipimo kizuri.
"Nina amini mchezo wetu na Mtibwa Sugar, utakuwa mzuri
, kutokana na ubora wa timu hiyo, ninajua itasaidia timu
yangu kupata mazoezi mazuri"alisema Logarusic.
Nae kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime, alisema ana
amini mchezo huo utakuwa mzuri kwake kutokana na
wapinzani wao kutoka katika mashindano.
Mexime alisema kuwa amepata nafasi ya kucheza na timu
kubwa, ambayo itampa mazoezi mazuri.
"Nina amini mchezo huo utakuwa mzuri kwangu kwa kuwa
nacheza na timu kubwa ambayo imetoka kwenye
mashindano"alisema Mexime.
Katika mchezo huo viingilio vitakuwa shilingi 20,000 VIP A,
shilingi 10,000 katika VIP B, wakati VIP C itakuwa shilingi
7,000 na sehemu ya viti vya orange na bluu itakuwa shilingi 5000.

No comments:

Post a Comment