Search This Blog

Thursday, January 16, 2014

GUNDOGAN: NITAFANYA MAAMUZI JUU YA HATMA YANGU NDANI YA DORTMUND


Kiungo wa Borrusia Dortmund anayewindwa na klabu ya Manchester United Ilkay Gundogan ameonya kwamba hatofanya haraka katika kuamua hatima yake ndani ya klabu ya Borussia Dortmund.

Gundogan, 23, atakuwa nje ya mkataba na Dortmund mwakani na Dortmund wapo katika harakati za kumuongezea mkataba mpya baada ya kuwapoteza Mario Goetze na Robert Lewandowski 
wakienda kwa mahasimu wao Bayern Munich. United pia wanamuwinda kiungo mwenye thamani ya  £40million Marco Reus.

David Moyes anaweza kukutana na upinzani kutoka kwa  Real Madrid ambao nao wanatajwa kumtaka Gundogan, ambaye ana thamani ya £25m, lakini kiungo huyo hajacheza tangu mwaka jana mwezi wa August kwa sababu ya maumivu ya mgongo na anasisitiza kwamba atachukua muda wake katika kuamua nini kinafuata katika maisha yake ya soka.

‘Bado suala hili lipo wazi,' aliiambia gazeti la Sport Bild. ‘Dortmund ndio kipaumbele cha kwanza. Nitafanya maamuzi kamili hivi karibuni lakini mpaka sasa sijaamua chochote.

‘Nitarudi katika ubora wangu. Naamini kipindi nilichokaa nje kimenifanya kuwa bora na imara zaidi. Lakini ni vigumu kutabiri lini hasa nitacheza tena.'

No comments:

Post a Comment