Search This Blog

Friday, January 31, 2014

DAKIKA ZA MWISHO ZA DIRISHA LA USAJILI: TETESI NA USAJILI ULIOKAMILIKA - MASAA MATANO YAMEBAKIA


Kim Kallstrom amekamilisha upimaji wa afya wa kujiunga na mkopo na Arsenal akitokea Spartak Moscow - wakati huo huo uhamisho wa mchezaji mkongwe wa kijerumani Miloslave Klose kuja Emirates umeshindikana rasmi.

Uhamisho wa beki Eliaqum Mangala na mwenzie Fernando kutoka umekwamba na wachezaji hao wameonekana kwenye ndege wakielekea jijini Madeira kwa ajili ya mechi ya Ligi ya Ureno kesho.

Papiss Cisse amekataa kujiunga na klabu ya Uturuki Trabzonspor lakini msenegal huyo bado anaweza kuuzwa usiku huu ikipatikana ofa ambayo Newcastle wanaitaka. 
Borussia Monchengladbach bado wanamhitaji mshambuliaji wa Newcastle.



Wilfred Zaha amejiunga rasmi na Cardiff City kwa mkopo akitokea Manchester United


Chelsea wamethibitisha kumsajili Kurt Zouma kutoka St Etienne, lakini mlinzi huyo ataendelea kubakia kwenye timu hiyo ya Ufaransa mpaka mwisho mwa msimu. 
Kinda hilo lenye miaka 19 amejiunga na Chelsea kwa mkataba wa miaka mitano na nusu. 
Emmanuel Frimpong amejiunga na Barnsley akitokea Arsenal

Kocha wa Manchester United amethibitisha rasmi kwamba wapenzi wa klabu hiyo wasitegemee kusajiliwa kwa mchezaji yoyote leo hii zaidi baadhi ya wachezaji wataondoka kwa mkopo.
Adel Taarabt amekamilisha usajili wake wa kujiunga na AC Milan akitokea QPR
Lewis Holtby amekamilisha uhamisho wake kutoka Tottenham kwenda Fulham kwa mkopo

No comments:

Post a Comment