Search This Blog

Tuesday, January 21, 2014

BARCELONA YATHIBITISHA KUTUMIA KIASI CHA PAUNDI MILIONI 495 KUUBORESHA UWANJA WA NOU CAMP.



Bodi ya wakurugenzi ya FC Barcelona imekataa wazo la kujenga kiwanja kipya na badala yake wamekubaliana kuongeza nguvu kuufanyia marekebisho uwanja wao wa Nou Camp.



Wanachama wa klabu ya FC Barcelona ambao kimsingi ndio wamiliki wa timu hiyo watapewa nafasi ya kupitisha wazo hilo la kuuboresha uwanja Wa Nou Camp kwa kupiga kura mnamo mwezi wanne mwaka huu kwenye mkutano mkuu wa wanachama wa klabu hiyo.



Kama wazo hilo litapitishwa na wanachama basi uwanja huo mkubwa kuliko viwanja vyote barani ulaya wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 98,000 kwasasa, utakuwa na uwezo wa kuingiza mashabiki 105,000 na kusaidia kuongeza kipato kutokana na vyanzo vya uwanja huo.  
Pia itakuwa fursa kwa mashabiki kuweza kuwaona wachezaji nyota ulimwenguni kama vile Lionel Messi na Neymar.



Mradi huo ambao pia unahusisha ujenzi wa kiwanja cha ndani cha mchezo wa kikapu pamoja na vitega ychumi vingine vingi unataraji kuighalimu kiasi cha paundi milioni 495 ambazo ni sawa na euro milioni 600.Kazi hiyo ya maboresho ya uwanja inataraji kuanza mwaka 2017 na inataria kumalizika mapema mwaka 2021.

Ili kufanikisha mradi huo Barcelona inategemea kuchukua mkopo benki wa kiasi cha paundi milioni 165,pia inategemea kupata kiasi cha paundi milioni 82 kutokana na haki za jina la uwanja huo na kiasi kingine kilichobaki cha pesa kitatokana na vyanzo vilivyopo hivi sasa.
Raisi wa klabu hiyo Sandro Rosell amesema wakati woote wa ujenzi michezo mbali mbali inayoihusu klabu hiyo itaendelea kuchezwa kwenye uwanja huo.

No comments:

Post a Comment