Search This Blog

Friday, December 13, 2013

HATIMAE SIMBA YAMALIZANA NA IVO MAPUNDA NA BEKI DONALD MOSOTI OMWANWA



Simba pia imemsainisha beki wa kati wa Gor Mahia Donald Mosoti Omwanwa,amesaini mkataba wa miaka miwili mbele ya katibu mkuu wa Simba Evodius Mtawala.



Donald Mosoti Omwanwa.....

 Ivo Mapunda akisaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Simba mbele ya katibu mkuu wa timu hiyo Evodius Mtawala.

3 comments:

  1. Vilabu vya Tanzani hasahasa Simba na Yanga, ni mafundi sana wa kubaini hazina ya ufundi na umaridadi wa mpira ulipo. Ila ni mahodari wa kuviua vipaji hivyo kirahisi. Huwezi kutegemea mbegu ya mpunga ichanue leoleo ufanikishe mavuno,ukiwa hivyo unakuwa hukumbuki ile falsafa ya mwenda pole.Ili tufike waliko TP Mazembe, Enyimba, na magwiji wengine Africa, hatuna budi kulea vipaji vyetu kwanza. Miaka michache iliyopita Tanzania walimwona Mapunda si lolote. Leo wanamwona mali baada ya kudondokewa na tone la CECAFA. watanzania anabidi tubadilike na mchezaji hana budi kupewa muda wa kutosha ili aoneshe mambo yake. Namwombea Mapunda afanikiwe Simba,ila awe mjanjamjanja manake wanamtindo wakubadilika muda wowote.

    ReplyDelete
  2. dah kaka Umesahau fadhila walizokufanyia wakenya? ama kwel sikio la kufa halisikii dawa simba watakufukuza kama hawakujui by seif mohamed korogwe tanga

    ReplyDelete
  3. Wewe Ivo vipi bwana.Kwa maoni yangu-Ungecheza hiyo CAF Champion League ukiwa na Gor Mahia,2014 uweze kuonekana kwa mawakala au nd'o umeridhika?,umefika mwisho wa mafanikio yako?.Sasa unakuja Simba ambao hawana uhakika sana wa kucheza CAF champion league 2015 ingawa ligi yetu bado inaendelea.Nimeona wachezaji wengi ULAYA wanagoma kusaini kwenda timu fulani kwa sababu timu hiyo haishiriki michuano ya UEFA champion league.Wewe ni mchezaji mkubwa lazima ungalie vitu kama hivyo not only a PAYROLL.Sipondi soka letu lakini..........!!!!

    David V

    ReplyDelete