Search This Blog

Monday, December 30, 2013

CAMEROON KWENDA BARANI ULAYA KUWASHAWISHI WACHEZAJI KURUDI KUITUMIKIA NCHI YAO


Ujumbe wa kutoka nchini Cameroon wanatarajiwa kwenye nchi Ulaya kuwashawishi wachezajiwa wa nchi hiyo wanachezea katika nchi za ulaya kujiunga na timu ya taifa ya nchi hiyo "Indomitable Lions".

Mpango huo wa kusaka vipaji vipya umekuja wakati Cameroon ikiwa inajiandaa kushiriki fainali za kombe la dunia mwaka kesho nchini Brazil.

Chama cha soka cha Cameroon - Fecafoot kimesema mpango wao kwa sasa ni kushawishi wachezaji wanne wanaocheza soka ya kulipwa nchini Ufaransa.

Wachezaji hao Axel Ngando anachezea klabu ya Auxerre ya ligi daraja la pili nchini Ufaransa, Samuel Umtiti anachezea Lyon na Jean- Christophe Behebeck anachezea Valenciennes.

Mchezaji mwinginie anayewindwa ili kuuongeza nguvu kwenye timu ya taifa ya Cameroon ni Paul Geoges Ntep de Madiba ambaye pia naye anayechezea Auxerre ya Ufaransa.

Tunataka kuwashawishi hao wachezaji wachezee timu ya taifa ya Cameroon, na hasa kwenye fainali za Kombe la Dunia na pia wachezee Cameroon kwa hapo baadae Shirikisho la soka la Cameroon limesema kwenye taarifa yake.

No comments:

Post a Comment