Search This Blog

Friday, November 22, 2013

ZIDAN APIGWA NYUNDO YA MIAKA SITA JELA


Mahakama moja nchini Misri imemuadhibu mchezaji wa zamani wa timu ya soka ya taifa hilo Mohamed Zidan kwenda jela kwa miaka sita baada ya kumkuta na hatia ya kutoa cheki tatu mbovu kwenye kampuni ya real estate.

Kampuni ya hiyo (Arab Company for Projects and Urban Development) ilifungua mashtaka dhidi ya Zidan, mapema mwaka huu.

Mwanasoka huyo, 31, amekuwa nje ya dimba tangu alipoondoka katika klabu ya Baniyas iliyopo huko UAE mwezi January mwaka huu. Zidan ambaye kwa sasa anafanya kazi ya uchambuzi katika TV ya Al-Jazeera Sports kama mchambuzi, ingawa bado hajatangaza kustaafu kabisa soka.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Dortmund na Werde Bremen hakuwepo mahakamani wakati hukumu hiyo ikitolewa.

No comments:

Post a Comment