Search This Blog

Thursday, November 14, 2013

RAISI WA BAYERN MUNICH AMWAGA CHOZI AKITANGAZA KUTENGENEZA FAIDA KUBWA ZAIDI KATIKA KIPINDI CHA MIAKA 113



Raisi wa Bayern Munich Uli Hoeness, anakabiriwa na kesi ya kukwepa kodi itakasomwa mwakani, jana alitokwa na machozi wakati akitangaza klabu yake kuvunja rekodi ya kuingiza mapato makubwa katika cha 113 years.
Katika mkutano wa mkuu wa klabu, Hoeness, ambaye alipokewa kwa shangwe, alishindwa kujizuia na kuanza kulia baada ya mabosi wenzie kumsifia kuiongoza vizuri timu hiyo na kupata mafanikio ya kushinda makombe matatu msimu uliopita. 
Hoeness, ambaye anashtakiwa kwa kushindwa kulipa kodi kutoka kwenye fedha zake zilizopo katika moja ya benki huko Uswis.
 
Hoeness, amekuwa katika klabu hiyo kwa zaidi ya miaka 40 kama mchezaji, kocha na saa raisi, alizungumzia matatizo yake ya kisheria, akisema kwamba alifanya makosa na kushindwa kulipa kodi kutoka kwenye akaunti yake ya nje.
'Nilifanya makosa kutokulipa kodi katika uwekezaji kutoka nje. Sikuchukua mamilioni ya fedha na kuyatoa nje ya nchi," alisema Hoeness, baada ya kujifuta machozi.  'Nitapambana na matatizo.'

'Nina imani kubwa na utawala wa kisheria wa Bavarian.
'Ninatumaini kwamba story hii itakuwa na mwisho mzuri mpaka kufikia mwezi  March. Na kama mpaka wakati huo nitaruhusiwa kuendelea kuwa hapa naahidi kuitumikia klabu hii mpaka pumzi yangu ya mwisho.'

No comments:

Post a Comment