Search This Blog

Monday, November 4, 2013

HATIMAE TORINO YAISIMAMISHA AS ROMA KWENYE SERIE A.



Katikati ya juma hili klabu ya AS Roma iliweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza kwenye historia ya Serie A kushinda michezo 10 mfululizo ya mwanzoni mwa msimu ilipoifunga Chievo bao 1-0.
Leo wameshindwa kuendeleza rekodi ya ushindi baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na timu ya Torino ugenini.
Roma walitangulia kufunga kupitia kwa kiungo mdachi Kevin Trootman kabla ya mchezaji wa zamani wa Roma Alessio Cerci hajaisawazishia Torino na kupelekea mchezo huo kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

No comments:

Post a Comment