Search This Blog

Saturday, November 30, 2013

ETHIOPIA YAITANDIKA ZANZIBAR HEROES 3-1

Zanzibar Heroes leo jioni imekubali kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Ethiopia katika mfululizo wa mchezo wa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Chalenji  uliopigwa katika Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya.

Jahazi za Heroes lilizamishwa na mabao ya Fasika Asfan dk 5, Salahadin Bargicho kwa mkwaju wa penalti dakika ya 37 baada ya Manaye Fantu kufanyiwa madhambi katika eneo la hatari na baadae Kebede alifunga la tatu dakika ya 83.

Kiungo mpya wa klabu ya Simba Awadh Juma Issa aliifungia bao la kufutia machozi Zanzibar. 

Kwa matokeo hayo, Zanzibar inabaki na pointi tatu na Ethiopia iliyoanza kwa sare ya bila kufungana na wenyeji Kenya, inakuwa na pointi nne.

1 comment:

  1. Sasa kazi kwa wenyeji..bado tuna matumaini

    ReplyDelete