Search This Blog

Tuesday, October 15, 2013

SERENGETI FIESTA SOCCER BONANZA SASA ZAMU YA DAR

Tamasha kubwa la Serengerti Fiesta Soccer Bonanza mwaka huu limeingia msimu wa tatu na limefanyika kwa mafanikio makubwa sana katika mikoa ya Kigoma,Singida,Morogoro,Mwanza na sasa ni zamu ya jiji la Dar Es Salaam.
Tamasha hilo linataraji kufanyika siku ya Jumamosi ijayo ya tarehe 19/10/203 kwenye viwanja vya Leaders kuanzia saa nne asubuhi.
Mashabiki wa vilabu vinane vya ulaya ( Manchester Utd,Chelsea,Liverpool,Arsenal,Real Madrid,Fc Barcelona,Ac Milan na Bayern Munich ) watapambana kumpata bingwa wa mkoa wa Dar Es Salaam.

Mashabiki wa Arsenal waliibuka washindi kwa changamoto ya mikwaju ya penati dhidi ya Manchester Utd kwenye uzinduzi wa bonanza la mwaka huu huko mkoani Kigoma, mkoani Singida mashabiki wa Liverpool wakafanikiwa kubeba ndoo baada ya kuwafunga mashabiki wa Bayern Munich mabao 2-0, huku mashabiki wa Chelsea wakiibuka mabingwa kwenye mikoa ya Morogoro na Mwanza.



No comments:

Post a Comment