Search This Blog

Friday, October 11, 2013

BARTON : FERGUSON ALIKUWA HANA UWEZO WA KUPANGA HATA KONI...



Kiungo mtukutu  wa Queens Park Rangers Joey Barton ameibuka tena kwenye vichwa vya vyombo vya habari baada ya kudai kocha wa zamani wa Manchester Utd Sir Alex Ferguso hakuwa na uwezo wa kufundisha,
Barton alidai nchini England mameneja wanathaminiwa sana kuliko makocha.

'Sina maana ya kutomuheshimu Sir Alex Ferguson - alikuwa meneja mkubwa lakini hakuwa na uwezo wa kufundisha,

sidhani kama alikuwa na uwezo wa kupanga hata koni. Kuna tofauti kubwa kati ya kocha na meneja'.

Barton pia amesema hakubaliani na wazo la kuundwa kwa tume ya kutafuta njia bora ya kuendeleza soka nchini England.
Akizungumza katika kilele cha mkutano wa Viongozi wa vilabu (Leaders in Sports ) uliofanyika kwenye uwanja wa Stamford Bridge , alisema: 'Timu ya taifa ya England ni mbovu na haiwezi kufanya vizuri hata kama itafuzu fainali za kombe la dunia mwakani nchini Brazil.

No comments:

Post a Comment