Search This Blog

Thursday, September 26, 2013

TIMU ZA WIZARA YA HABARI ZAANZA KWA KUTOA VIPIGO SHIMIWI

Wachezaji wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakiwa wamembeba Naibu katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Ole Sante Gabriel kusherehekea ushindi walioupata timu za kuvuta kamba za wizara hiy 
Mshambuliaji wa timu ya mpira wa pete Hadija Jaha akijiandaa kutoa pasi kwa mwenzake wakati walipokutana na timu ya Wizara ya Maji. Wizara ya Habari ilishinda kwa alama 19 kwa 15.

Kiungo wa timu ya mpira wa pete ya Wazara ya Habari Flora Mwakasala akijiandaa kutoa pasi kwa mshambuliaji wa timu hiyo Grace Kinga

Kiungo wa timu ya mpira wa miguu ya Wizara ya Habari Mbozi Katala akimtoka beki wa timu ya Wizara ya Maji wakati timu hizo zilipokutana katika mshindano ya SHIMIWI.Habari ilishindwa kwa 1-0.
Wachezaji wa timu ya kuvuta kamba ya Wanawake ya Wizara ya Habari wakiivuta timu ya Afrika Mashariki (haipo pichani) katika mchezo wa mashindano ya SHIMIWI Septemba 22.

Wachezaji wa timu ya kuvuta kamba ya Wanawake ya Wizara ya Habari wakiivuta timu ya Afrika Mashariki (haipo pichani) katika mchezo wa mashindano ya SHIMIWI Septemba 22.

Nahodha wa timu ya soka ya Wizara ya Habari Carlos Mlinda akiongoza wenzake kusalimiana na wachezaji wa timu ya Wizara ya Maji wakati walipokutana katika ya kwanza ya mashindano ya SHIMIWI.

Wachezaji wa timu ya kuvuta kamba ya Wanaume ya Wizara ya Habari wakiivuta timu ya Afrika Mashariki (haipo pichani) katika mchezo wa mashindano ya SHIMIWI Septemba 22.

Kikosi cha mpira wa miguu cha Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. 
Kikosi cha mpira wa pete cha Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.

No comments:

Post a Comment